• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI KWA KUTOA ELIMU KWA WAKINAMAMA

Posted on: August 11th, 2020


Katika kuadhimisha wiki ya unyonyeshaji Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kupitia kitengo cha lishe, imetoa mafunzo kwa wakinamama juu ya swala zima la lishe na utaratibu wa unyonyeshaji kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano na zaidi ili kuepuka na maradhi ya utapiamlo na udumavu.


Mafunzo hayo juu ya unyonyeshaji na lishe yalitolewa na afisa lishe wa Manispaa ya Ilemela Bi Paulina Everest Machango wakati akizungumza na wanawake waliokuja kliniki ya watoto katika zahanati ya Nyerere na kituo cha afya Buzuruga.


Bi Paulina amewataka wakinamama hao kuhakikisha wanatoa kipaumbele katika kunyonyesha maziwa ya mama pekee bila aina nyingine yeyote ya chakula kwa watoto wa chini ya miezi sita ili kuwakinga watoto hao dhidi ya magonjwa ya utapiamlo na udumavu huku akisisitiza kuhakikisha wanawapatia mlo kamili watoto wote wenye umri wa zaidi ya miaka miwili ili waweze kuwa na afya njema na imara

“Wamama wengi tuna watoto wenye utapiamlo ule wa kati kitu ambacho ni hatari maana tukizembea kidogo wanaanza kuugua wanalazwa, na hii yote ni kwasababu ya unyonyeshaji na ulishaji, usiofaa kwa mtoto” ,Alisema


Aidha Bi Paulina alikemea mila potofu na tabia zisizofaa zinazochangia udumavu kwa watoto ikiwemo kuwazuia kula baadhi ya vyakula muhimu na utandawazi mbovu kwa wakinamama wa kuogopa kunyonyesha inavyotakiwa watoto wao wakikwepa kudondoka kwa maziwa katika vifua vyao.


Kwa upande wake muuguzi wa kituo cha afya Buzuruga Bi Grace Msabaha ametaja faida mbalimbali zinazopatikana kwa kufuata utaratibu mzuri wa unyonyeshaji ikiwemo kupata mtoto mwenye afya na kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo utapiamlo, kuimarisha mahusiano baina ya mtoto na mzazi pamoja na kutumika kama njia ya uzazi wa mpango kwa kipindi cha miezi sita ya mwanzo katika ukuaji wa mtoto.

Bi Sarafina Isaac ni mmoja ya mama aliyehudhuria kliniki ya elimu ya unyonyeshaji na lishe anaeishi mtaa wa Buzuruga, ameshukuru kwa elimu iliyotolewa na wataalamu hao huku akiwasihi wamama wenzake kuzingatia utaratibu wa kunyonyesha na lishe kwa watoto ili kujenga kizazi kilichokuwa salama na chenye afya bora katika jamii.

Maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 1 hadi 7 ya mwezi wa nane yakiwa na lengo la kusisitiza umuhimu wa kulinda, kuimarisha na kuendeleza unyonyeshaji wa maziwa ya mama na pia kuweka msukumo wa kipekee katika kuunganisha nguvu ya wadau mbalimbali ili kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Kwa mwaka 2020 maadhimisho haya yalibeba kauli mbiu ya "Tuwawezeshe Wanawake Kunyonyesha  kwa Afya Bora na Ulinzi wa Mazingira"


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.