• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

HUDUMA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUCHOCHEA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

Posted on: September 5th, 2025

Dhima kuu ya mkakati wa kitaifa wa nishati safi ya kupikia (2024-2034) uliozinduliwa mwezi Mei 2024 na Rais Samia Suluhu Hassan inalenga kuhakikisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia iliyo nafuu, endelevu, salama na rahisi kutumika,ukilenga kutoa mwongozo wa namna ya kupunguza athari za kiafya, mazingira na kuboresha maisha ya wananchi huku ukipunguza athari ya mabadiliko ya tabia nchi

Katika kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan , za kuhakikisha watanzania wanaachana na matumizi ya nishati isiyo safi na salama, Wilaya ya Ilemela nayo imeendelea kuhamasisha utumiaji wa nishati safi yakupikia katika taasisi zake ambapo mnamo tarehe 26 Agosti 2025, Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 zilizindua huduma hii ya nishati safi ambayo imeleta ahueni kwa wanafunzi sambamba na wapishi  

"Awali tulikuwa tunaumwa vifua, macho, mafua kutokana na moshi wa kuni  lakini kwa sasa kutokana na nishati hii mbadala mazingira ni masafi hakuna tena moshi hivyo wanafunzi nao  watarajie chakula kisafi kitaiva kwa wakati",anasema Amos Stanley

Amos stanley ni mpishi wa shule ya sekondari Buswelu, ameshukuru kwa mradi wa nishati safi ambao umefanikisha kufanya kazi katika hali ya usafi na usalama , chakula kinaiva vizuri na kwa wakati.

Nao wanafunzi wa Buswelu Sekondari wameshukuru kwa nishati hii mbadala kwani imewasaidia wao kuwahi masomo kutokana na kwamba chakula kinaiva kwa wakati kufuatia uwepo wa jiko hili la nishati safi hivyo wameishukuru serikali kwa kampeni hii ambayo pia inasaidia utunzaji wa mazingira 

"Zamani wapishi walikuwa wanachukua muda mrefu kupika  kwa sababu ya matumizi ya kuni hivyo kuwapelekea kuchelewa masomo yao, lakini sasa kufuatia uwepo wa nishati mbadala inasaidia, nishati mbadala imesaidia kupunguza uchafuzi wa mazingira, nishati mbadala imetusaidia kuweka mazingira katika hali ya usafi na salama"

Akizindua huduma hiyo ya matumizi ya nishati safi  katika shule ya sekondari Buswelu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Ndg. Ismail Ussi amepongeza Wilaya kwa jitihada za kuhakikisha matarajio ya Mhe Rais yanafikiwa 

"Kufuatia matumizi ya nishati safi tunaona kuwa jengo limetumika lakini bado ni safi hii ni kwa sababu ya nishati safi ambayo tunatumia, ambayo imesaidia juu ya utunzaji wa mazingira na mimi naamini kuwa walio wengi wataendelea kuthamini na kukumbusha jamii juu ya matumizi ya nishati safi huku akiwataka vijana kuwa mabalozi wazuri wa kampeni hii", alisema Ndg Ussi 

Katika Wilaya ya Ilemela jumla ya taasisi 61 zinatumia nishati safi ya kupikia kati ya taasisi 256 zilizopo sawa na asilimia 23.8. Hata hivyo, malengo ya Wilaya ni kufikia asilimia 80 ifikapo mwaka 2034. Taasisi hizo ni Shule za Msingi na Sekondari za Umma na Binafsi, Vyuo na Hoteli. Pia Wilaya imegawa jumla ya majiko 1725 ya nishati safi ambapo 1700 yaligawiwa kwa mama lishe na majiko 25 yaligawiwa kwa walengwa wa TASAF. 

Matumizi ya nishati safi­ ya kupikia ni agenda mahususi ambayo imechukua nafasi kubwa katika Sera, Mipango na Mikakati ya Serikali mbalimbali duniani. Umuhimu wa agenda hii unasukumwa na ongezeko la uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi pamoja na athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya nishati isiyo salama ya kupikia. 

Announcements

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • ELIMU YA LISHE YATOLEWA KW WATOA HUDUMA ZA AFYA ILEMELA

    September 15, 2025
  • MAAFISA USAFIRISHAJI NA WAVUVI WAASWA KUTOTUMIKA VIBAYA KIPINDI CHA UCHAGUZI MKUU 2025

    September 11, 2025
  • MAASKARI 121 WA JESHI LA AKIBA WAHITIMU MAFUNZO WAASWA KUVIISHI VIAPO VYA

    September 09, 2025
  • VIJANA WAMEHIMIZWA KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI KATIKA MAENEO YAO KUJIKWAMU KIUCHUMI

    September 05, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.