• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

HATI 315 ZA ARDHI ZAKABIDHIWA KWA WATUMISHI ILEMELA

Posted on: August 17th, 2020

Watumishi wa Manispaa ya Ilemela wakiwemo walimu wa shule za msingi na sekondari pamoja na watumishi kutoka idara ya afya wamekabidhiwa hati miliki 315  za ardhi ambapo hati 297 zimekabidhiwa kwa walimu na hati 18 zimekabidhiwa kwa watumishi wa idara ya Afya.

Hati hizo zilikabidhiwa na Naibu waziri wa wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi Mhe Dkt Angeline Mabula ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa Manispaa hiyo wa kutoa motisha kwa walimu kutokana na juhudi walizofanya katika ufundishaji na kuwawezesha wanafunzi wa Manispaa ya Ilemela kufanya vizuri katika mitihani ya Taifa kwa darasa la saba, kidato cha nne na sita kwa mwaka 2018 ikiwa ni pamoja na kuhakikisha watumishi wake wanapata makazi kwa gharama nafuu.


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Naibu Waziri wa Ardhi Mhe Dkt Angeline Mabula mbali na kuipongeza halmashauri ya manispaa ya Ilemela kwa uhodari wake katika zoezi la urasimishaji makazi, upimaji na umilikishaji aliwataka watumishi hao kuzitumia hati hizo kwa shughuli za maendeleo.


“Ilemela imekuwa ikifanya vizuri katika mambo mbalimbali ikiwemo sekta ya elimu, mtakumbuka hata mwaka jana ilikuwa ya pili kitaifa, Sisi kama serikali tunaona jitihada zenu ndio maana tumetoa utaratibu rahisi wa kuwapatia viwanja kwa walimu wetu ili kuweza kuwapatia motisha katika kazi” Alisema

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya ardhi na mipango miji Ndugu Shukran Kyando alisema kuwa hati hizo zilizotolewa kwa walimu ni sehemu ya viwanja 525 ambavyo vipo kwenye mpango huo wa mradi wa viwanja vya walimu katika eneo la Nyamiswi Kata ya Sangabuye Manispaa ya Ilemela.

Katibu wa kamati ya mradi wa viwanja hivyo, Mwalimu Albert Mahuyu alisema kuwa pamoja na  kamati yake kukutana na changamoto mbalimbali wakati wa uendeshaji wa zoezi hilo, alimshukuru aliyekuwa Mbunge wa Ilemela Mhe. Angelina Mabula kwa kuja na wazo hilo la kutoa motisha ya viwanja kwa walimu pamoja na uongozi mzima wa Manispaa chini ya Mkurugenzi John Wanga kwa namna ambavyo walihakikisha kuwa zoezi hilo linafanikiwa.


Nao wanufaika wa mradi huo wa viwanja wamemshukuru aliyekuwa Mbunge wa Ilemela Dkt. Angeline Mabula pamoja na uongozi wa Manispaa ya Ilemela kwa kuwaheshimisha walimu kwa kuweza kupata hati kwa ajili ya kujenga nyumba katika maeneo rasmi hivyo hiyo ni fursa hata wakistafuu kuishi maisha mazuri huku wakishauri  Halmashauri nyingine nchini ziweze kuanzisha mradi kama huo ili kuwawezesha walimu na watumishi wengine kuwa na uhakika wa maisha hata watakapo staafu.


Jumla ya Hati 1,596 zilitolewa kwa wananchi mbalimbali wa Manispaa ya Ilemela, wakiwemo walimu na watumishi wa idara ya Afya hii ikiwa ni muendelezo wa ugawaji wa hati na kufanya jumla ya hati zilizotolewa kipindi cha mwaka 2020 kuwa 6,061.












Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.