• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Fedha zikatumike kwa malengo yaliyokusudiwa: MKurugenzi Ilemela

Posted on: October 18th, 2021

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Mhandisi Modest Apolinary amewataka watendaji katika kata ya Nyamanoro kuhakikisha wanatumia fedha za ujenzi wa madarasa mapya kwa malengo yaliyokusudiwa.

Ameyasema hayo alipokuwa katika ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo katika kata ya Nyamanoro huku akiwataka wananchi wa kata hiyo kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuboresha mazingira ya upatikanaji wa huduma za kijamii ikiwemo uboreshaji wa sekta ya elimu.

'.. Tumeshawawekea kwenye akaunti yenu milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mapya mawili, Mkatumie fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa ..' Alisisitiza

Aliendelea kufafanunua kuwa fedha hizo kiasi cha shilingi milioni arobaini zimetolewa na Serikali Kuu kupitia mpango wa matokeo kutokana na ufanisi (EP4R) kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mawili ya shule ya msingi Mkudi kata ya Nyamanoro ili kuweka mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia.


Pamoja na hayo, Mhandisi Modest amesema kuwa kupitia mapato ya ndani shule za msingi Mkudi na Mji Mwema zimetengewa kiasi cha shilingi milioni saba na laki tano kila moja kwa ajili ya  ukamilishaji wa madarasa yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ikiwa ni mchango wa halmashauri katika kuunga mkono nguvu za wananchi wake.


Kwa upande wake Diwani wa kata ya Nyamanoro Mhe Maganiko Ngaka  mbali na kuishukuru Serikali kwa kutoa fedha za ujenzi wa miundombinu ya elimu katika kata yake amempongeza mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela kwa kufika katika kata yake na kutembelea maeneo ya kata yake kusikiliza kero na changamoto zinazowakabiki wananchi wake huku akiahidi kuendelea kushirikiana nae katika kuwaleta maendeleo wananchi wa kata hiyo


Nae Mkuu wa shule ya msingi Mkudi Bi Zuhura Ally Bilal amemshukuru mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela kwa kutoa fedha za ujenzi wa madarasa mapya na kumalizia yale ya awali kwani kitendo hicho kitasaidia kupunguza changamoto iliyokuwa ikiwakabili kwa muda mrefu ya upungufu wa vyumba vya madarasa


Katika ziara hiyo Mhandisi Modest alipata fursa ya kuzungumza na watumishi wa kata hiyo pamoja na kukagua miradi ya barabara, elimu na masoko.




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.