• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utumishi na Utawala
        • Mipango na ufuatiliaji
        • Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Elimu Sekondari
        • Elimu ya Awali na Msingi
        • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
        • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Miundombinu na Uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Vitengo
        • Mazingira na Usafishaji
        • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
        • Michezo, Utamaduni na Sanaa
        • Fedha na Uhasibu
        • Sheria
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Manunuzi
        • TEHAMA na Takwimu
        • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ELIMU YA MATUMIZI BORA YA FEDHA YATOLEWA KWA WANUFAIKA WA MKOPO WA ASILIMIA 10

Posted on: January 18th, 2023

Jumla ya vikundi 37 vinavyonufaika na mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri ya manispaa ya Ilemela inayojumuisha asilimia 4 kwa ajili ya wanawake,asilimia 4 kwa vijana na asilimia 2 kwa watu wenye ulemavu vimepatiwa mafunzo sambamba na zoezi la ujazaji wa mikataba ya mikopo ambayo inatarajiwa kutolewa katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023.



Akizungumza wakati wa zoezi la kujaza mikataba na utiaji saini wa mikataba ya ukopeshaji fedha  kwa  vikundi hivyo lililofanyika katika ukumbi  wa manispaa ya Ilemela Afisa maendeleo wa manispaa ya Ilemela Bi Amina Bululu amewataka wana vikundi hao kuhakikisha wanatumia fedha hizo kwa ajili ya miradi iliyokusudiwa sanjari na kuhakikisha wanarejesha fedha hizo katika muda uliopangwa kulingana na mkataba bila riba yeyote.


“ Ni utaratibu wetu wa kawaida kutoa mafunzo haya ya kukumbushana matumizi bora ya fedha mnazokopeshwa hasa tunapokutana kwa pamoja kama hivi ili zilete tija katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mnazofanya na kufanya zoezi la kukopesha liwe endelevu.”



Aidha Bi. Bululu amevipongeza vikundi vya wanawake kwa marejesho mazuri ya fedha hizo za mkopo huku akiviasa vikundi vya vijana na watu wenye ulemavu kuhakikisha navyo vinarejesha kwa wakati ili viweze kupata fedha nyingi zaidi na kukuza biashara sambamba na kuongeza kipato chao.



Kwa upande wake afisa maendeleo ya vijana manispaa ya Ilemela Bi Lucy Nicholaus Matemba amevitaka vikundi vinavyokopeshwa na manispaa kuhakikisha vinayaishi makubaliano yaliyo katika mkataba pamoja na kusisitiza kuwa wasiache kuwatumia maafisa maendeleo walio katika maeneo yao au wale wa makao makuu ya wilaya pindi zinapojitokeza changamoto zozote.


Monika Makaranga ni mwenyekiti wa kikundi cha Tupendane group 2020 kilichopo Msumbiji kata ya Kawekamo kinachojishughulisha na ufugaji wa kuku ,usindikaji wa vyakula ambavyo ni viungo na unga wa lishe,kwa niaba ya kikundi chake ameishukuru Manispaa ya Ilemela kwa kukubali kuwapatia mkopo awamu nyingine wa shilingi milioni 10 ambayo wanatarajia kuitumia kwa mradi mpya wa bajaji.



Nae Bi. Judith Kasuja Joseph ambae ni mlemavu wa miguu kutoka kata ya Kahama mtaa wa Isela ameipongeza manispaa hiyo kwa uwepo wa masharti mepesi upande wa walemavu katika kupata mkopo.



Halmashauri ilitenga jumla ya kiasi cha shilingi milioni 285,000,000 inayotarajiwa kutolewa kwa vikundi 37 ndani ya manispaa ya Ilemela kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023.





Announcements

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2022 SHULE ZA SERIKALI NA BINAFSI MANISPAA YA ILEMELA January 29, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA September 30, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KATIKA KIPINDI CHA ROBO YA KWANZA JULAI-SEPTEMBA 2022 October 11, 2022
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA ILEMELA LAHIMIZA USHIRIKIANO KATI YA SEKTA BINAFSI NA ZA UMMA

    March 18, 2023
  • JAMII YA ILEMELA YATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    March 11, 2023
  • WANANCHI ILEMELA WAPONGEZWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    March 11, 2023
  • WADAU WA MAENDELEO WAENDELEA KUUNGUA JUHUDI ZA SERIKALI

    March 02, 2023
  • Tazama zaidi

Video

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA TAUSI
More Videos

Quick Links

  • Kuhakiki Taarifa za Mpiga Kura
  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip
  • Maombi ya leseni ya biashara

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.