• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ELIMU YA LISHE NA NJIA BORA ZA UNYONYESHAJI YATOLEWA KWA WAKINAMAMA ILEMELA

Posted on: August 11th, 2022

Elimu ya Lishe sambamba na njia bora za unyonyeshaji imeendelea kutolewa kwa jamii ya Ilemela hususan wakina mama wanaonyesha na wanaotarajiwa kujifungua.

Wakina  mama hao wametakiwa kujali lishe bora kwa familia zao hasahasa kwa kina mama wanaonyesha na watoto ambao wapo katika hatua za ukuaji kwa kuzingatia kuwa uimara na ubora wa akili ya mtu mzima huanza kutengenezwa kwa viwango pindi mtu anapokuwa mdogo kwa kupitia lishe anayopata kwa wakati huo.


Akitoa elimu hiyo ya lishe na namna ya unyonyeshaji bora kwa wakina mama waliohudhuria kliniki zao za kawaida katika kituo cha afya Buzuruga, Muuguzi Bi Asteria Athanas amewakumbusha kuwa, lishe bora ni kula mlo kamili na wa kutosha wenye mchanganyiko wa viini lishe vyote vinavyotakiwa mwilini kutoka makundi matano ya vyakula ambayo ni wanga, protini, sukari na mafuta pamoja na vitamin na madini.


Wakinamama hao wamepata fursa ya kufahamu mambo mbalimbali kuhusu lishe ikiwa ni pamoja na faida za unyonyeshaji kwa watoto wachanga maziwa ya mama pekee kuanzia umri wa 0 hadi miezi 6, ambapo huboresha ukuaji, uimarisha kinga ya mwili kwa mtoto na kuboresha mahusiano baina ya mama na mtoto.


Bi Asteria akizitaja faida za unyonyeshaji mzuri amesema kuwa ni pamoja na kupunguza uwezekano wa kuwa na uzito uliozidi au kiriba tumbo kwa mtoto na kumfanya kuwa na akili nzuri huku akisisitiza kuwa jukumu la kupata lishe bora kwa familia sio la mama peke ake bali ni la wanafamilia wote.


Nae Damaris Dawson ambae ni muuguzi wa kituoni hapo amewataka kina mama kuwaongezea lishe zaidi watoto baada ya miezi sita kwani itamfanya mtoto akue vizuri na kumrahisishia mama kuendelea na majukumu yake mengine ya uzalishaji kiuchumi.


Judith Mgeta na Pili Kilanda ni wakina mama waliofika katika kituo hicho cha Afya cha Buzuruga wamewashukuru wataalam kwa kazi kubwa ya kuelimisha jamii juu ya masuala mbalimbali ya afya hususan elimu hiyo ya lishe bora na njia bora za unyonyeshaji huku wakiomba elimu hiyo iendelee kuwafikia wengi zaidi


“Tunaishukuru sana serikali yetu hususan Manispaa yetu ya Ilemela kwa kuweka utaratibu huu wa sisi kina mama kupata elimu mbalimbali kama hizi hatujasoma lakini tunaweza kupata uelewa wa vitu vingi vya afya kupitia mikusanyiko kama hii ,tunaomba utaratibu huu uendelee na kuwafikia wakinamama wengi zaidi, kwani ni msaada mkubwa mno kwetu” Wamesema



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.