• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC MASALA 'Wapuuzeni wanaotaka mtoke maeneo rasmi ya biashara'

Posted on: May 6th, 2022

Wafanyabiashara ndogo ndogo maarufu kwa jina la machinga wametakiwa kuwapuuza wanasiasa wanaowashawishi kutoka katika maeneo rasmi yaliyotengwa na Serikali kwaajili ya kufanyia biashara zao.


Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Elias Masala wakati akizungumza na wafanya biashara wa masoko ya Kabwaro, Buzuruga, Nyasaka na Kiloleli wakati wa ziara yake ya kutembelea masoko hayo kwaajili ya kusikiliza kero, changamoto na maoni ya wafanyabiashara juu ya utekelezaji wa shughuli za kila siku tangu kutengwa kwa maeneo rasmi ya biashara baada ya agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hasan la kutenga maeneo rasmi na rafiki kwaajili ya shughuli za kibiashara ambapo amewataka wafanya biashara wadogo kushirikiana na Serikali katika kutatua changamoto zinazowakabili, kuweka mazingira rafiki ya biashara ili kujikwamua kiuchumi badala ya kurudi katika maeneo hatarishi yasiyofaa kwa shughuli za biashara jambo linalorudisha maendeleo nyuma.


‘.. Wapo watu wasiowatakia mema wanapita kuwashawishi mrejee katika maeneo hatarishi tuliowatoa hapo awali, Msikubali Serikali yenu ni sikivu itaendelea kushirikiana nanyi kutatua kero zote zinazowakabili mkiwa hapa hapa sokoni, atakaetoka nje ya soko lililotengwa na Serikali kitakachompata shauri yake ..’ Alisema


Aidha Mhe Masala amewahakikishia wafanya biashara hao kuwa Serikali itaendelea kuboresha maeneo yao ya kibiashara ikiwemo kuweka miundombinu ya barabara, umeme, maji, vyoo na kudhibiti vitendo vya kiharifu ili waweze kufanya biashara kwa amani na utulivu huku akiwataka kuendelea kuiunga mkono Serikali yao katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kimaendeleo.


Kwa upande wake mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Joseph Apolinary amefafanua kuwa manispaa yake imetenga fedha kwaajili ya ukarabati wa miundombinu ya masoko na itaendelea kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanya biashara hao huku akiahidi kutengeneza barabara ya soko la Nyasaka hivi karibuni ili iweze kufikika kwa urahisi.

Abdulrahman Simba ni diwani wa kata ya Nyasaka amemshukuru mkuu wa wilaya ya Ilemela kwa kutembelea masoko ya kata yake huku akiwaasa wananchi wa kata yake kuhakikisha hawatoki nje ya maeneo rasmi yaliyotengwa na Serikali kwa shughuli za biashara ndogo ndogo.


Akihitimisha Bwana Samuel Mwita mfanyabiashara kutoka soko la Nyanda Nyasaka kwa niaba ya wafanyabiashara wengine wa soko hilo amelalamikia wizi kwa njia ya kishirikina unaofanyika katika soko hilo baina ya wafanyabiashara maarufu kama ‘chuma ulete’ huku akitaka viongozi kutafuta ufumbuzi juu ya kero hiyo inayowasababishia hasara na kufilisika mitaji yao .

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.