Watumishi wa umma wametakiwa kutoa huduma bora kwa wananchi pamoja na kuacha kuwajibu lugha za kejeli ili kuepusha chuki baina yao na serikali
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Elias Masala wakati wa kikao chake cha kusikiliza kero za wananchi alichokifanya katika viwanja vya mtaa wa Kabambo kata ya Kiseke ambapo amewataka watoa huduma katika ofisi za umma kuhakikisha wanaacha kutumia lugha chafu na kebehi kwa wananchi huku akiwaasa kutanguliza ukarimu wanapo hudumia wananchi
‘.. Kutisha wananchi wanaofata huduma katika ofisi za umma haikubaliki, Serikali inaonekana katili, haiwajali watu kumbe sababu ya watu kujibu hovyo wananchi, Mkiwahudumia vibaya wataichukia Serikali yao ..’ Alisema
Aidha Mhe Masala ameiagiza mamlaka ya maji safi na maji taka jijini Mwanza MWAUWASA kumchukulia hatua mfanyakazi wake anaelalamikiwa na wananchi wa kata hiyo kwa kutoa lugha chafu, kejeli na unyanyasaji pamoja na kuomba mrejesho katika ofisi yake juu ya hatua za kinidhamu atakazochukuliwa mtumishi huyo
Kwa upande wake msaidizi wa meneja wa MWAUWASA wa kanda inayohudumia kata ya Kiseke Michel Mayani amefafanua kuwa pamoja na msisitizo wa ukusanyaji wa kodi za maji kwa wananchi, Mamlaka yake inakemea huduma mbovu kwa wananchi na kwamba itamchukulia hatua mtumishi wake anaelalamikiwa sanjari na kuwaomba wananchi hao kulipa ankara za maji kwa wakati.
Mkuu wa wilaya ya Ilemela anaendelea na kliniki ya utatuzi wa kero za wananchi katika maeneo mbalimbali ya wilaya yake akiambatana na wakuu wa idara za manispaa ya Ilemela, wakuu wa taasisi za Serikali zinazofanya kazi ndani ya wilaya yake ikiwemo TANESCO, MWAUWASA, TARURA na siku ya kesho atakuwa kata ya Kirumba kusikiliza wananchi wa kata hiyo
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
Postal Address: 735 MWANZA
Telephone: + 255 736 200910
Mobile:
Email: md@ilemelamc.go.tz
Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.