• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC MASALA ASISITIZA UWEKEZAJI KATIKA ELIMU

Posted on: July 26th, 2022

“Kama unaona elimu ni gharama basi jaribu ujinga”, ni maneno ambayo ameyanukuu Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe Hasan Masala wakati akikabidhi madawati kwa shule za msingi za Ilemela.

“Sisi tumeona tusijaribu ujinga lazima tuwekeze katika elimu ambayo imegawanyika katika makundi mbalimbali kuanzia elimu ya awali hadi ya chuo kikuu na ili kuwa na Taifa lenye watu wenye kuelewa wajibu wao ni lazima tuwekeze kwao angali wachanga”, amesisitiza


Mhe Masala ameongeza kwa kusema kuwa Ushirikiano ndio nguzo pekee katika kufanikisha kila jambo ambalo tunapanga kufanya kwa pamoja, jamii nzima ya Ilemela tunalo jukumu la kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya sita kwa kushiriki kwa namna mbalimbali katika shughuli za kujiletea maendeleo.

Pamoja na hayo amewashukuru wadau mbalimbali ambao kwa namna moja au nyingine wameshiriki katika kufanikisha upatikanaji wa madawati hayo 1500


“Nitoe shukrani zangu za dhati kwa uongozi wa Halmashauri na wadau wote walioshiriki kutufikisha hapa tulipo leo kwa kujitoa kwenu kupatikana kwa kiasi hiki cha madawati, lengo letu lilikuwa ni kupata madawati 1000 kwa awamu ya kwanza lakini tumevuka lengo kwa asilimia 50 hii yote ni katika kumuunga mkono Rais wetu Mhe.Samia Suluhu Hassan kuboresha sekta ya elimu.Tujivunie watoto wetu wanapokuwa katika mazingira mazuri ya kupata elimu kwani hata ufaulu utaongezeka.” Amesema Masala.

Ameongeza kwa kusema kuwa jitihada hizi za maboresho katika sekta ya elimu zinaendelea katika ngazi ya Wilaya na mkoa ambapo amebainisha kuwa tayari mkoa wa Mwanza umeanza oparesheni kabambe ya kuondoa upungufu wa madarasa lengo ikiwa ni kupunguza na kuondoa kabisa changamoto ya uchache wa vyumba vya madarasa ndani ya mkoa mzima wa mwanza.


Nae Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela Mhe.Renatus Mulunga ameshukuru wananchi na wadau wote waliofanikisha upatikanaji wa madawati hayo kama moja ya njia ya kurahisha ukaaji mzuri wa mpangilio.


“Taifa lolote duniani likipata elimu hakika maendeleo yanapatikana,yote haya yamewezekana kwa sababu ya ushirikiano mkubwa wa uongozi wa Ilemela na  wadau mbalimbali wa maendeleo,hatutochoka kusema tunashukuru sana na ninaomba ushirikiano huu uendelee katika kuijenga Ilemela yetu.” Amesema Mhe.Mulunga

Daniel Andrew, na Juliana Anthony ni wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Buswelu ambayo ni moja ya shule iliyonufaika na ujio wa madawati hayo 1500 wametoa shukrani kwa niaba ya wanafunzi wote wa Ilemela kwa wote waliofanikisha upatikanaji wa madawati haya kwani utaenda kuondoa adha ya wanafunzi hao kukaa chini hivyo kuongeza ufaulu katika masomo yao, huku wakitoa ahadi ya kusoma kwa bidii ili kufikia malengo waliyojiwekea.


“Sisi wanafunzi wa Ilemela tunatoa shukrani zetu za dhati kwa uongozi wa juu wa  serikali kuanzia kwa Mhe.Samia Suluhu Hassan na ngazi zote za chini,tunaahidi kusoma kwa bidii na kuzidi kuthamini juhudi hizi zinazofanywa na serikali na wadau mbalimbali wa elimu.  

Niendelee kuisisitiza jamii na kuwaomba kuendelea kuunga mkono jitihada hizi za kuchangia miundo mbinu kama madawati na vyumba vya madarasa zaidi katika kuhakikisha watoto wanasoma na kukaa katika mazingira rafiki amesema Bi Jamila  Khalfan ambae ni Kaimu Afisa Elimu Msingi Manispaa ya Ilemela


Upatikanaji wa madawati haya 1500 kwa shule za msingi 17 ni matokeo ya harambee iliyofanyika tarehe 31/05/2022 iliyokuwa na lengo la kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati katika shule za msingi za Ilemela.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.