• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC MASALA AITAKA JAMII YA SANGABUYE KUSHIRIKI SHUGHULI ZA MAENDELEO

Posted on: September 13th, 2023

Mhe Hassan Elias Masala ameitaka jamii ya Sangabuye kuhakikisha inashiriki kwa kuchangia nguvu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo hususan ujenzi wa zahanati ya Sangabuye unaoendelea na kusisitiza kuzingatia ubora na ufanisi wa ujenzi wa zahanati hiyo.


Ametoa kauli hiyo alipokuwa katika ziara ya kikazi ya ukaguzi wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea katika kata hiyo ambapo alipata fursa ya kukagua ujenzi wa zahanati mpya inayojengwa katika kata ya Sangabuye kupitia fedha za mradi wa kunusuru kaya maskini TASAF.


Aidha Mhe Masala amekemea ubadhirifu wa vifaa vya ujenzi vitakavyoletwa kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo na kwamba Serikali haitamvumilia mtu yeyote atakaeiba au kuhujumu kwa namna yeyote ile utekelezaji wa mradi huo uweze kufika tamati


‘.. Hatutaki mgogoro katika utekelezaji wa mradi huu, wananchi tunaowajibu wa kuhakikisha tunashiriki kwa asilimia mia, kwa kufuata miongozo na taratibu za utekelezaji wa mradi huu, Fedha ikipotea hapa hakuna maneno mimi natia pingu’ Alisema


Nae mratibu wa mradi wa kunusuru kaya masikini TASAF wilaya ya Ilemela Leonard Robert amesema kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika baada ya miezi  mitatu kutoka sasa na kwamba changamoto kubwa iliyokuwa ikiukabili ambayo kwa sasa imeshatatuliwa ni kuchelewa kufunguka kwa mifumo ya malipo ya benki kuu hivyo kushindwa kufanya malipo


Gabriel Remmy ni mhandisi wa manispaa anaesimamia mradi huo ambapo amesema kuwa mpaka sasa mradi huo umefikia asilimia 15 kwa jengo la wagonjwa wa nje na asilimia 10 kwa jengo la nyumba ya mtumishi huku akiahidi kuusimamia mradi huo kwa ufanisi na umakini ili lengo lililokusudiwa liweze kutimia


Mhe Renatus Mulunga Mstahiki Meya wa manispaa ya Ilemela ambae pia ni diwani wa kata ya Sangabuye mbali na kumshukuru mkuu huyo wa wilaya kwa kuitembelea kata yake amefafanua kuwa kero kubwa inayoikabili kata yake kwa sasa ni changamoto ya upatikanaji wa uhakika wa  maji safi na salama, upatikanaji wa umeme na mtandao hivyo kuomba kushirikiana na mkuu huyo wa wilaya kwaajili ya kuzipatia ufumbuzi wa kudumu.


Ujenzi wa zahanati hiyo ya Sangabuye unatarajia kutumia kiasi cha shilingi Milioni 149 hadi kukamilika ambapo majengo yanayojengwa ni pamoja na jengo la wagonjwa wan je (OPD), jengo la kitengo cha chanjo (RCH) na nyumba ya mtumishi .





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.