Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Elias Masala amefungua mafunzo ya jeshi la akiba maarufu kama mgambo tukio lililofanyika siku ya Jumanne Septemba 12, 2023 katika viwanja vya Lumala sekondari .
Mhe.Masala amesema mafunzo hayo ni muhimu kwa vijana kwani yanalenga kuwatengeneza kuwa wazalendo kwa nchi yao.
"Mafunzo haya yanawatengeneza kijitegemea,kuwa wazalendo na kupambana mazingira yenu kwa hali zote."
Nae Luteni kanali Evans Akili ambaye ni Mshauri wa jeshi la akiba Wilaya ya Ilemela amefafanua umuhimu wa mafunzo hayo ikiwa ni pamoja na vijana wanaohitimu kuwa chachu ya ulinzi na usalama ndani ya jamii.
"Tutaendelea kuwanoa vijana hawa wawe wazalendo kweli kweli na wawe bidhaa hadhimu yenye manufaa kwa nchi yetu." Amesema Luteni kanali Evans
Hamida Kiduma ni mmoja wa wanafunzi wa jeshi la akiba waliojiandikisha mwaka huu yeye anasema anashukuru serikali kwa kuanzisha kozi hiyo kwani imekuwa mkombozi kwa vijana wengi kama njia ya kutafuta pa kutokea.
" Naambiwa mazoezi ni magumu lakini ntakomaa,naona urahisi wa kupata ajira nikimaliza hapa na pia ntaweza kujisimamia katika maamuzi ya kijitegemea kimaisha."
Jumla ya wanafunzi 97 wa mafunzo ya askari wa akiba wamejiandikisha mwaka huu 2023 ndani ya Wilaya ya Ilemela ambapo mafunzo hayo yatachukua miezi mitatu.
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
Postal Address: 735 MWANZA
Telephone: + 255 736 200910
Mobile:
Email: md@ilemelamc.go.tz
Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.