• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC MASALA AAGIZA WANAFUNZI WOTE KURIPOTI SHULE

Posted on: January 17th, 2024

Mhe Hassan Masala Mkuu wa wilaya ya Ilemela amefanya ziara ya kikazi iliyokuwa na lengo la kukagua hali ya mahudhurio ya wanafunzi wa kidato cha kwanza na darasa la kwanza sambamba na ukaguzi wa mialo ikiwa ni pamoja na kufikisha taarifa ya ugonjwa wa kipindupindu  katika kata za Kayenze, sangabuye, bugogwa


Akikagua maendeleo ya mwenendo wa kuripoti kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza, darasa la kwanza na awali, Mhe Masala, amewataka wazazi kuhakikisha watoto wanaripoti shule sambamba na kuwalinda watoto hao dhidi ya matendo ya kikatili huku akipiga marufuku ya watoto wenye umri wa kwenda shule kufanya kazi hususan muda wa masomo.


“Watoto ni wa kwetu sote na jukumu la kuwasomesha na kuwalinda ni letu sote kwani watoto ni mali ya jamii” amesema


Aidha amewataka  wanafunzi kuwafikishia ujumbe wanafunzi wenzao ambao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza na hawajaripoti shule kuhakikisha wanaripoti shule kwani masomo yameshaanza na hakutakuwa na marudio.


“Waambieni waje shule, kwa ambao hawajakamilisha mahitaji ya shule kama vile sare, madaftari wafike shule wakiwa na sare za shule za msingi hadi watakapopata lengo ni kuhakikisha wote mnasoma kwa pamoja na pia nasisitiza kuwa hakuna mchango wowote ambao utamuondoa mwanafunzi shule”


Pamoja na hayo Mhe Masala amewahimiza wanafunzi hao kuhakikisha wanasoma na kuacha kukimbilia mambo mengine huku akiwataka kuwa mabalozi wa kusemea umuhimu wa elimu


“Wanafunzi msome, mjali sana elimu kwa sababu ndicho kimewaweka hapa elimu ni kila kitu, tumezungukwa na jamii ambayo bado inatakiwa kujua umuhimu wa elimu msikimbilie maisha kila jambo lina wakati wake.”



Ziara hiyo ilienda sambamba na ukaguzi wa hali ya usafi wa mialo na kuongea na wavuvi na kuwafikishia taarifa ya ugonjwa wa Kipindupindu ambapo amewataka kuzingatia  matumizi sahihi ya vyoo yakienda sambamba na matumizi ya maji safi  na salama kwa  kuweka maji safi ya kunawa pamoja na sabuni na  kuhakikisha wananchi wananawa  ili kuweza kuepukana na maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu.


Aidha Mhe Masala, amewataka Mama lishe kuzingatia usafi wa mazingira katika maeneo wanapopika vyakula vyao. Kwa kuchukua  tahadhari kwani wasipokuwa makini unaweza kutokea mlipuko wa kipindupindu, huku akiwataka maafisa afya wafanye jitihada za kukagua maeneo mapishi yanafanyika na pindi watakapokuta mama lishe hakidhi vigezo vya kutoa huduma kufunga biashara zao kwani kwa kufanya hivyo ndio usalama wa wananchi/walaji.


“Mazingira lazima yawe masafi maji yanayotumika yawe masafi, majiko yawe masafi, kupunguza uwepo wa nzi na tule chakula ambacho ni cha moto”, alisistiza Mhe Masala.


“Ni wajibu wetu kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu kama wana mwanza hivyo  Kila mmoja awe mlinzi na msimamizi wa mwenzake, hili ni jukumu letu sote.”Alihitimisha.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • "TUUFANYE USAFI KUWA NI TABIA YA KUDUMUA": ANNA MBAO

    May 31, 2025
  • WATAALAM WA MANISPAA YA ILEMELA WAJENGEWA UWEZO MATUMIZI YA MFUMO WA MANUNUZI WA UMMA

    May 29, 2025
  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.