• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utumishi na Utawala
        • Mipango na ufuatiliaji
        • Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Elimu Sekondari
        • Elimu ya Awali na Msingi
        • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
        • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Miundombinu na Uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Vitengo
        • Mazingira na Usafishaji
        • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
        • Michezo, Utamaduni na Sanaa
        • Fedha na Uhasibu
        • Sheria
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Manunuzi
        • TEHAMA na Takwimu
        • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC MASALA AAGIZA UFUATILIAJI KWA WANAFUNZI AMBAO HAWAJARIPOTI

Posted on: February 6th, 2023

Mhe. Hassan Masala, Mkuu wa wilaya ya Ilemela amewataka maafisa elimu watendaji, viongozi wa kata na mitaa kwa kushirikiana na wazazi, kufanya ufuatiliaji wa haraka kwa wanafunzi 1500 ambao hawajaripoti shule ili kuweza kuhakikisha watoto wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2023 wanaripoti shuleni.


Agizo hilo amelitoa wakati wa kikao kazi cha kutathimini hali ya uandikishaji wa darasa la awali na la kwanza na hali ya kuripoti kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa mwaka 2023 ambapo amewataka viongozi na watendaji kushirikiana pamoja kuhakikisha watoto ambao hawajaripoti wanaripoti ndani ya wiki mbili.


Aidha Mhe Masala mbali na kumshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa fedha za ujenzi wa madarasa amekemea dhana potofu  iliyojengeka kwa jamii kwamba hakuna sababu ya kusoma kwa kuwa ajira ni changamoto hivyo akatumia wakati huo kuwaasa wataalam na viongozi kutoa elimu kwa wazazi wasioelewa juu ya umuhimu wa elimu huku akihimiza kuwekeza katika elimu.


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela, Mhe. Renatus Mulunga amempongeza Mhe Masala kwa kuendelea kuweka msisitizo juu ya suala la Elimu kwani anaamini maendeleo yoyote hupatikana kupitia elimu huku akihimiza kuwajali walimu wanaofanya kazi katika maeneo ya pembezoni kwa kuwaboreshea mazingira ya kuishi

Kwa upande wake mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Apolinary ametaja mafanikio yaliyofikiwa kwa muda mfupi ndani ya sekta ya elimu ikiwemo ujenzi wa shule mpya tano za sekondari, ujenzi wa shule saba mpya za msingi, pamoja na ukamilishaji wa maboma 40 ya vyumba vya madarasa yanayosubiria kupauliwa pamoja na kuahidi milioni tano kwa shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya kidato cha nne mwaka huu sambamba na kuwataka wenyeviti wa mitaa kuongeza juhudi za ukusanyaji wa mapato ili Serikali iweze kuboresha zaidi sekta hiyo.

Tathmini hiyo ilienda sambamba na utoaji wa vyeti kwa viongozi mbalimbali kwa ajili ya kutambua michango yao katika sekta ya Elimu, ambapo Mkuu wa Wilaya aliwatunuku vyeti hivyo, wenyeviti wa mitaa, watendaji kata na mitaa, wakuu wa shule , Mkurugenzi, Mstahiki Meya  pamoja na Mbunge wa jimbo la Ilemela huku akiwashukuru kwa utayari wao katika kusimamia miradi ya elimu.




Announcements

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2022 SHULE ZA SERIKALI NA BINAFSI MANISPAA YA ILEMELA January 29, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA September 30, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KATIKA KIPINDI CHA ROBO YA KWANZA JULAI-SEPTEMBA 2022 October 11, 2022
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA ILEMELA LAHIMIZA USHIRIKIANO KATI YA SEKTA BINAFSI NA ZA UMMA

    March 18, 2023
  • JAMII YA ILEMELA YATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    March 11, 2023
  • WANANCHI ILEMELA WAPONGEZWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    March 11, 2023
  • WADAU WA MAENDELEO WAENDELEA KUUNGUA JUHUDI ZA SERIKALI

    March 02, 2023
  • Tazama zaidi

Video

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA TAUSI
More Videos

Quick Links

  • Kuhakiki Taarifa za Mpiga Kura
  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip
  • Maombi ya leseni ya biashara

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.