• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utumishi na Utawala
        • Mipango na ufuatiliaji
        • Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Elimu Sekondari
        • Elimu ya Awali na Msingi
        • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
        • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Miundombinu na Uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Vitengo
        • Mazingira na Usafishaji
        • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
        • Michezo, Utamaduni na Sanaa
        • Fedha na Uhasibu
        • Sheria
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Manunuzi
        • TEHAMA na Takwimu
        • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC ILEMELA APIGA MARUFUKU MICHANGO KIDATO CHA KWANZA

Posted on: January 17th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Elias Masala amekataza michango ya aina yeyote itakayosababisha wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2023 washindwe kuripoti shuleni.


Agizo hilo amelitoa leo wakati wa ziara yake kwa shule za msingi na sekondari ndani Manispaa ya Ilemela yenye lengo la kufuatilia mahudhurio ya kidato cha kwanza, awali na darasa la kwanza, kusikiliza changamoto za walimu na kuhamasisha ufaulu ambapo amewataka wakuu wa shule, maafisa elimu na viongozi wa mitaa na kata kuhakikisha watoto wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza wanaripoti mashuleni na kwamba hakuna kuzuia mtoto yeyote kuingia darasani

‘.. Kuna wazazi mnawazuia eti sababu hawajajaza fomu za kujiunga na shule kwenye kile kipengele cha daktari, wengine kwa kukosa sare, wengine sijui hawana jembe. Nasema marufuku kuzuia watoto kwasababu ya michango yeyote ..’ Amesema


Aidha Mhe Masala mbali na kumshukuru na kumpongeza Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hasan kwa ujenzi wa madarasa, viti na meza ametaka kuchukuliwa hatua wazazi  watakaoshindwa kupeleka watoto shuleni pamoja na watendaji watakaokwamisha zoezi la wanafunzi kuripoti shuleni.

Akimkaribisha mkuu huyo wa wilaya, Mwakilishi wa afisa elimu sekondari manispaa ya Ilemela Mwl Alex Mkusa amewapongeza walimu kwa kazi kubwa wanayoifanya kuhakikisha manispaa ya Ilemela inaendelea kushika nafasi nzuri kitaifa huku akiwataka kuongeza juhudi katika ufundishaji ili ufaulu kwa nafasi na daraja la ufaulu viende sambamba (GPA)


Kwa upande wake diwani wa kata ya Mecco Mhe Godlisten Kisanga amewaasa viongozi wa mitaa kushirikiana kuhakikisha watoto wote wanaripoti shuleni sanjari na kuahidi ufuatiliaji wa nyumba kwa nyumba ili kubaini watoto waliochaguliwa na hawajaripoti mashuleni

Jumla ya wanafunzi 12,507 wamepangwa kuripoti shuleni kwa mwaka wa masomo wa 2023 ndani ya wilaya ya Ilemela ambapo mpaka sasa wanafunzi 6367 pekee ndio waliokwisha ripoti mashuleni sawa na asilimia 53 ya wanafunzi wote huku wanafunzi 6140 wakiwa hawajaripoti


Announcements

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2022 SHULE ZA SERIKALI NA BINAFSI MANISPAA YA ILEMELA January 29, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA September 30, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KATIKA KIPINDI CHA ROBO YA KWANZA JULAI-SEPTEMBA 2022 October 11, 2022
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA ILEMELA LAHIMIZA USHIRIKIANO KATI YA SEKTA BINAFSI NA ZA UMMA

    March 18, 2023
  • JAMII YA ILEMELA YATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    March 11, 2023
  • WANANCHI ILEMELA WAPONGEZWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    March 11, 2023
  • WADAU WA MAENDELEO WAENDELEA KUUNGUA JUHUDI ZA SERIKALI

    March 02, 2023
  • Tazama zaidi

Video

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA TAUSI
More Videos

Quick Links

  • Kuhakiki Taarifa za Mpiga Kura
  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip
  • Maombi ya leseni ya biashara

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.