• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DAS ILEMELA ASISITIZA LISHE BORA

Posted on: October 31st, 2024

Katibu tawala wa Wilaya ya Ilemela wakili Mariam Msengi amewataka wananchi wa Ilemela kuzingatia lishe bora katika ulaji wao wa kila siku huku akisisitiza umuhimu wa taifa kuwa na wananchi wenye afya nzuri katika kuijenga nchi.

Akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya lishe katika mtaa wa Nyambiti uliopo kata ya Buzuruga wakili Msengi amesema serikali ya awamu ya sita inaendelea kuweka juhudi kubwa katika kuhakikisha kuwa wananchi wake wanapata huduma bora za afya kwa kuimarisha miundo mbinu mbalimbali ya sekta ya afya ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vituo vya kutolea huduma hizo ndani ya Manispaa hiyo huku mkazo wa utoaji elimu ya lishe ukiendelea.

"...Kina mama sisi ndo viongozi wa familia katika mambo haya,tuwe mstari wa mbele kuzingatia lishe bora kwa familia zetu..."

Akitoa taarifa wakati wa maadhimisho hayo Afisa lishe wa Manispaa ya Ilemela Bi.Pili Khasim amesema takwimu za mwaka 2023/2024 zinaonyesha asilimia 30 ya watoto wenye umri chini ya miaka mitano wamedumaa, asilimia 12 wana uzito pungufu na asilimia 3 wana ukondefu sambamba na hali duni kwa wanawake walio katika umri wa kuzaa (mwaka 15 - 49).

"...tunayo mafanikio tangu kuanzishwa kwa mpango wa lishe kitaifa ikiwemo kuongezeka kwa mwitikio wa jamii kuhudhuria elimu za lishe na kuleta watoto kupata nyongeza ya matone ya vitamin A na dawa za minyoo ambapo lengo lilikuwa watoto 66,381 na tukapata watoto 66,711 sawa na asilimia 100.4..." amesema Pili.

Nae diwani wa kata ya Buzuruga Mhe.Manusura Sadick Lusigalie amewataka wananchi wake kuunga mkono serikali ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuzingatia ulaji sahihi wa makundi yote muhimu ya vyakula ili kuleta nguvu kazi yenye matokeo chanya kwa taifa.

Scola Chacha ni mkazi wa mtaa wa Nyambiti yeye anashukuru wataalam hao kwa elimu walioipata na kuahidi kuwa balozi mzuri kwa wananchi wenzake.

Huduma zilizotolewa wakati wa maadhimisho hayo ni pamoja na kipimo cha HIV na sukari, chanjo mbalimbali kama polio,chanjo zote za watoto,matone ya vitamini A na dawa za minyoo na kipimo cha urefu na uzito wa mwili sambamba na jiko darasa.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.