• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BUKOBA DC WAJIFUNZA NONDO ZA SEKTA YA UVUVI ILEMELA

Posted on: December 12th, 2024

Wataalam na waheshimiwa madiwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba wamefanya ziara Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kwa lengo la kujifunza shughuli za ukusanyaji wa mapato na kuona namna ambavyo Manispaa ya Ilemela imekuwa ikifanikiwa katika shughuli zake mbalimbali za maendeleo hasa sekta ya uvuvi hali inayosababisha ukuaji wa kasi wa Manispaa hiyo.

Akisoma taarifa ya makusanyo ya vyanzo vya mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 Afisa mapato wa Halmashauri hiyo Theogenes Laurent amesema kwa mwaka wa fedha 2023/2024 halmashauri ilipanga kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni 14.4 hadi kufikia tarehe 30 Juni 2024 jumla ya shilingi Bilioni 13.6 zilikusanywa sawa na 94.8% ya lengo la bajeti huku Halmashauri hiyo ikipanga kukusanya kiasi cha shilingi Bilioni 14.9 kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo mpaka sasa imekusanya 40.31% ya lengo kwa mwaka huu wa fedha.

Ivon Maha ni Afisa uvuvi katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela amewaambia wageni hao kuwa uwekezaji mkubwa katika maeneo ya mialo unaweza kusaidia kuongeza mapato ya mazao ya uvuvi.

“..Manispaa ya Ilemela inashuhudia maendeleo makubwa ya uwekezaji katika sekta ya uvuvi kwa kujenga na kuboresha miundombinu ambapo mialo inaendelea kuboreshwa,ujenzi wa viwanda vikubwa vinne vya kuchakata samaki na uanzishwaji wa viwanda vidogo 12 kwa ajili ya mazao ya uvuvi,vitalu nyumba vya kukaushia dagaa na masoko ya kisasa.” Amesema Maha

Ameongeza kuwa mafanikio katika sekta ya uvuvi yametokana na maboresho ya zana za uvuvi kama nyavu na boti sambamba na elimu ya matumizi yake kwa wavuvi,mikopo kwa ajili ya wavuvi inatolewa na utolewaji wa elimu ya ufugaji wa samaki kupitia mabwawa na vizimba shughuli ambayo imeongeza uzalishaji wa mazao ya samaki kwa matumizi ya majumbani na biashara.

“..Hongereni sana kwa kazi nzuri mnayoifanya,tuna vingi tumejifunza na ni lazima tuvifanyie kazi naomba mkurugenzi uridhie maombi yetu ya kuomba wataalam wako kuja kwetu kutuelekeza zaidi juu ya mengi tuliyoyaona hapa..”Amesema Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Bukoba Mhe.Privatus Mwoleka.

Nae Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Bi.Neema Semwaiko amepokea pongezi nyingi zilizotolewa na wageni hao huku akikiri kuwa inatia moyo katika utendaji kazi na inachochea ari ya kufanya vizuri zaidi .

“..Halmashauri yetu ipo tayari kushirikiana na ninyi kwa namna ambavyo kwa pamoja tutaona inafaa na inaleta tija lengo ni kuhakikisha tunafanya kazi ili kuleta maendeleo kwa jamii zetu tunazozitumikia.”

Akihitimisha kusanyiko hilo Mstahiki meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Mhe.Renatus Mulunga amesema ushirikiano ndio nguzo pekee katika kufanikisha mipango yote,ameongeza kuwa Manispaa ya Ilemela inafanya kazi kwa nguvu ya utatu ambapo yupo mbunge,serikali na wananchi.

“.. Halmashauri yoyote ili iendelee ni lazima kukusanya mapato,kikubwa ni elimu kutolewa kwa wahusika na sheria ziwepo na zisimamiwe kwa wale watakaokwenda tofauti wachukuliwe hatua..”

Maeneo yaliyotembelewa ni mwalo wa Kayenze ndogo uliopo kata ya Bugogwa na soko la samaki la kimataifa Kirumba ndani ya kata ya Kirumba.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.