• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utumishi na Utawala
        • Mipango na ufuatiliaji
        • Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Elimu Sekondari
        • Elimu ya Awali na Msingi
        • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
        • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Miundombinu na Uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Vitengo
        • Mazingira na Usafishaji
        • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
        • Michezo, Utamaduni na Sanaa
        • Fedha na Uhasibu
        • Sheria
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Manunuzi
        • TEHAMA na Takwimu
        • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BILIONI 61.3 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO ILEMELA

Posted on: May 15th, 2023

Serikali imetoa zaidi ya shilingi Bilioni 61.3 kwa ajili ya kutekeleza  miradi ya maendeleo ndani ya manispaa ya Ilemela katika sekta ya afya, elimu na  miundo mbinu mbalimbali.

Hayo yamebainishwa na mstahiki meya wa manispaa ya Ilemela Mhe. Renatus Mulunga wakati wa kikao cha baraza la madiwani kwa ajili ya  kupokea na kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa kipindi cha robo ya tatu inayoanza Januari hadi Machi, 2023.

Aidha Mhe.Mulunga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hasan kwa kutoa fedha hizo huku akilipongeza baraza la madiwani la Ilemela kwa kupata hati safi inayotokana na usimamizi na matumizi sahihi ya fedha za maendeleo.

“ Naendelea kuishukuru Serikali kwa fedha inazoleta kutekeleza maendeleo, tuendelee kuwaombea viongozi wetu hasa Mhe Rais na Mbunge kwa juhudi zao za kuchochea maendeleo, Rais anatoa fedha nyingi sana katika miradi tunayotekeleza ..’ Alisema

Aidha Mhe Mulunga amemshukuru mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Apolinary  kwa jitihada zake za ukusanyaji wa mapato zinazochochea utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja na kuwataka madiwani kuunga mkono juhudi hizo

Kwa upande wake mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Apolinary amefafanua kuwa mpaka sasa manispaa yake imeshakusanya  kiasi cha shilingi 12,189,314,578 sawa na  asilimia 90 ya makisio ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kati ya mapato halisi ya shilingi 11,943,338,632 ambayo ni sawa na asilimia 92 ya bajeti.

Nae Diwani wa kata ya Pasiansi Mhe Rosemary Mayunga amempongeza mkurugenzi wa Ilemela na watumishi wote kwa mchango wao katika kuhakikisha manispaa hiyo inapata hati safi huku Diwani wa kata ya Mecco Mhe Godlisten Kisanga akisema kuwa hakuna manispaa inayopata hati safi kama kuna matumizi yasiyo sahihi ya fedha za umma hivyo kuwaasa wananchi kuendelea kushirikiana na viongozi wa maeneo yao katika kutekeleza shughuli za maendeleo.

Manispaa ya Ilemela inaendelea na utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo katika maeneo yake huku kukiwa na usimamizi wa matumizi sahihi wa fedha za miradi ya maendeleo kwa zaidi ya miaka kumi na kupata hati safi katika vipindi vyote.

Announcements

  • TANGAZO LA BODI YA MFUKO WA ELIMU July 20, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 KWA SHULE ZA SEKONDARI ZA MANISPAA YA ILEMELA July 13, 2023
  • TANGAZO KWA UMMA KUKUMBUSHWA KULIPA VIWANJA June 23, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA AFISA MTENDAJI WA MTAA (II) June 20, 2023
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RC MAKALLA AWATAKA WATENDAJI KUTATUA KERO ZA WANANCHI

    September 19, 2023
  • GESI NISHATI MBADALA RAFIKI WA MAZINGIRA: MHE MABULA

    September 16, 2023
  • WANANCHI WA ILEMELA WAMETAKIWA KUFANYA USAFI KUWA AJENDA YA KUDUMU

    September 16, 2023
  • RC MAKALLA AIPONGEZA ILEMELA UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST

    September 14, 2023
  • Tazama zaidi

Video

WITO WATOLEWA KWA WANAFUNZI WALIORIPOTI KIDATO CHA TANO SHULE ZA ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Kuhakiki Taarifa za Mpiga Kura
  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip
  • Maombi ya leseni ya biashara

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.