• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BILIONI 2.7 ZATUMIKA KUKAMILISHA KIVUKO CHA MV ILEMELA

Posted on: January 9th, 2020

Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni mbili na milioni mia saba kukamilisha ujenzi wa Kivuko cha MV ILEMELA kitakachokuwa kinafanya safari zake Kutoka Kisiwa cha Bezi kuja Kayenze wilayani Ilemela ili kutatua adha ya muda mrefu iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa wilaya hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa wizara ya ujenzi, uchukuzi na mawasiliano mheshimiwa Ashanta Nditiye wakati wa zoezi la uingizaji wa kivuko hicho majini, zoezi lililoendeshwa katika karakana ya Kampuni ya utengenezaji wa meli ya Ms Songoro Marine iliyopo kata ya Ilemela ambapo alisema kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Mhe Dkt John Magufuli imedhamiria kuimarisha sekta ya usafirishaji na kutatua adha mbalimbali zinazowakabili wananchi kwa kutenga fedha kwaajili ya ujenzi wa vivuko 21 vipya na kukamilika kwa kivuko cha Mv Ilemela kinakamilisha idadi ya vivuko 31 nchi nzima  kwa vipya na vya zamani.

‘..  Ndugu zangu Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni mbili nukta saba kuhakikisha kivuko hiki kinakamilika na mpaka sasa tumeambiwa zaidi ya asilimia 98 imeshakamilika na leo tunakiingiza majini kwa mara ya kwanza  ...’ Alisema

Aidha kuhusu ajali mbalimbali zinazojitokeza nchini hasa ndani ya ziwa viktoria ameziagiza mamlaka zinazohusika kuhakikisha zinazuia ajali hizo kwani zipo ambazo si za lazima zinazosababishwa na uzembe wa baadhi ya wataalamu wakiwemo madereva wasiokuwa na ujuzi wakutosha hivyo kuiagiza TASAC kufanya uchunguzi wa manahodha wa vyombo vya majini kabla ya kukabidhiwa vyombo vya usafiri.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe John Mongella aliishukuru Serikali na Rais Magufuli kwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo ndani ya mkoa wake ikiwemo ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza, ujenzi wa Vivuko, ujenzi wa hospitali mpya mbili za wilaya ile ya Isanzu Ilemela na ya Buchosa, ukarabati wa hospitali ya mkoa Sekou Toure na ile ya rufaa ya Bugando huku akiwataka wananchi kuendelea kumuombea mheshimiwa Rais na kumuunga mkono.

Akihitimisha Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt. Angeline Mabula ameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kumaliza adha ya usafiri ya muda mrefu iliyokuwa ikiwasumbua wananchi wa jimbo lake hasa wa maeneo ya Kayenze waliokuwa wakitaabika na suala la usafiri kwenda Kisiwa cha Bezi huku akiomba kuanza mapema kwa safari za kivuko hicho ili wananchi hao wasiendelee kuteseka sanjari na kuomba kupatiwa ufumbuzi kwa kero ya mawasiliano inayowakabili wananchi wa maeneo ya Sangabuye ombi ambalo lilipokelewa na naibu waziri wa uchukuzi na kumuagiza mkurugenzi wa mamlaka ya mawasiliano kanda ya ziwa kushughulikia suala hilo.





Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • AWAMU YA KWANZA UCHANJAJI MIFUGO KUANZA TAREHE 03 JULAI, KUKU ELFU 70 KUCHANJWA

    July 02, 2025
  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.