• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BILIONI 2.67 KUTENGENEZA BARABARA ZA ILEMELA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

Posted on: February 10th, 2023

Takriban kiasi cha shilingi Bilioni 2.67 kinatarajiwa kutumika kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Wilaya ya Ilemela katika mwaka wa fedha 2023/2024.


Hayo yamebainishwa na meneja wa TARURA Wilaya ya Ilemela Mhandisi Sobe Makonyo wakati akiwasilisha mapendekezo ya bajeti ya mpango wa matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2023/2024 katika baraza la Madiwani la Manispaa ya Ilemela.


Mhandisi Sobe ameviainisha vyanzo vikuu vya fedha za matengenezo ya barabara katika utekelezaji wa kazi za matenegezo, ukarabati na ujenzi wa barabara kuwa ni mfuko wa matengenezo ya barabara, mfuko wa maendeleo ya barabara tozo na Jimbo.  pamoja na  wafadhili wengine kama Benki ya Dunia ambao hutekeleza miradi kwa kushirikiana na TARURA.


Kwa upande wa fedha za Mfuko wa Barabara amesema kuwa fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 1.17 kimetengwa kwa ajili ya matengenezo na ujenzi wa barabara huku chanzo cha fedha za tozo kikiwa kimetengewa kiasi cha shilingi bilioni moja na chanzo cha mfuko wa jimbo kimetengewa kiasi cha Shilingi Milioni mia tano fedha hizo zikiwa ni  kwa ajili ya matengenezo na ujenzi wa barabara katika mwaka wa fedha 2023/2024.


Aidha, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Ofisi ya TARURA Wilaya ya Ilemela imependekeza kujenga Barabara ya Kahama-Igogwe-Isanzu-Kabusungu (Ilemela Hospital road) 2.0km kwa kiwango cha lami nyepesi na barabara ya Mkudi (0.6km) kwa kiwango cha mawe kwa kutumia chanzo cha Mfuko wa Maendeleo ya Barabara  na hii ni endapo tu bajeti hiyo itaridhiwa na kupitishwa katika ngazi za juu amesema Mhandisi Sobe

Wakichangia bajeti hiyo Waheshimiwa Madiwani wameshauri kuwa TARURA ijielekeze zaidi katika barabara ambazo zimekua korofi na zenye changamoto za muda mrefu hususani maeneo ya milimani ambapo wameshauri zijengwe barabara za mawe maeneo kama vile kitangiri,Kirumba,Nyamanoro na Ibungilo


“Jiografia ya Ilemela eneo kubwa imetawaliwa na milima, tujipange kwenye ujenzi wa barabara za mawe hasa maeneo ya miinuko kwani barabara za mawe ndio zinadumu kwa kipindi kirefu”, amesema Mhe Donald Ndalo diwani wa Kata ya Kitangiri akichangia bajeti hiyo.


Aidha waheshimiwa madiwani wameishauri TARURA kuwa, maeneo ya kuelekea kwenye taasisi kama vile zahanati,shule ,masoko na maeneo ya huduma za jamii barabara zake zifanyiwe matengenezo ya mara kwa mara.


Nae Mhandisi Sobe ameahidi ushirikiano na Manispaa ya Ilemela kwa ajili ya kujenga barabara ya kiwango cha lami kuelekea hospitali ya wilaya iliyopo Isanzu


Kwa mujibu wa takwimu za barabara zilizohakikiwa na wizara ya ujenzi, mtandao wa Barabara unaosimamiwa na TARURA Wilaya ya Ilemela una urefu wa km 875.85 Kati ya Mtandao mzima wa Barabara, Barabara za Lami ni km 37.16 sawa na (asilimia 4.24) Zege ni km 1.904(asilimia 0.22) Mawe Km 4.98 (asilimia 0.57) Changarawe ni km 92.03 (asilimia 10.51) na Udongo ni km 739.783 (84.46 asilimia).



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.