• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BILIONI 1.2 KUJENGA SHULE MBILI ZA SEKONDARI NA NYUMBA

Posted on: August 1st, 2024

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imepokea jumla ya kiasi cha shilingi Bilioni 1,268,560,418.00 kutoka serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili mpya za sekondari, Masemele sekondari katika kata ya Shibula na Kilabela sekondari katika kata ya Bugogwa pamoja na ujenzi wa nyumba moja ya walimu katika shule ya sekondari Kisenga iliyopo kata ya Kiseke.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Bi.Ummy Wayayu wakati akiwasilisha taarifa ya shughuli zilizotekelezwa na ofisi yake katika mkutano wa baraza la madiwani kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo amefafanua kuwa ujenzi wa kila shule utagharimu kiasi cha shilingi Milioni 584.2 sambamba na ujenzi wa nyumba moja kwa gharama ya shilingi Milioni 100 itakayogawanyishwa mara mbili “2 in 1” kwa ajili ya waalimu wawili kuishi.

“ Fedha hizi zilipokelewa mwishoni mwa mwaka wa fedha uliopita na taratibu za kutambua maeneo ujenzi utakakofanyika zinaendelea na tunatarajia utekelezaji wake utakamilika mara moja .”

Aidha Bi. Wayayu amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuleta fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali ndani ya manispaa yake huku akiwaomba viongozi wenzake kuendelea kushirikiana katika kusimamia matumizi bora ya fedha hizo kwenye maeneo yao.

Nae Mbunge wa Ilemela Mhe.Dkt.Angeline Mabula mbali na kumpongeza Mkurugenzi huyo kwa taarifa nzuri ya utekelezaji amesema kuwa serikali kupitia ombi lake bungeni  imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya ufundi itakayojengwa kata ya Bugogwa na shule mpya ya msingi itakayojengwa kata ya Shibula na kuwaomba madiwani kushirikiana katika maendeleo.

“ Wataalam wetu naomba muanze kuwaza ujenzi wa shule za ghorofa ,ardhi haiongezeki ila watu wanaongezeka .” Amesema mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela Mhe.Renatus Mulunga.

Diwani wa kata ya Nyakato Mhe.Jonathan Mkumba amepongeza taarifa ya Mkurugenzi iliyoonyesha mgawanyo mzuri wa fedha katika kila kata kwa ajili ya miradi mbalimbali ya Maendeleo.

Sarah Shija ni mkazi wa mtaa wa Buswelu ni mmoja wa wananchi waliohudhuria mkutano huo wa baraza la madiwani yeye anapongeza jitihada za uboreshaji wa miundo mbinu ya elimu inayofanywa na Manispaa .

Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

    June 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.