• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BENKI YA DUNIA YARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI ILEMELA

Posted on: September 18th, 2024

Mtaalam kutoka Benki ya dunia ndugu Aquiline Safari akiambatana na wataalam kutoka wizara ya elimu sayansi na teknolojia na OR-TAMISEMI amefanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya elimu ya SEQUIP katika shule za sekondari na BOOST katika shule za msingi ndani ya Manispaa ya Ilemela.

Safari amesema lengo la ziara hiyo ni kufanya tathimini ya manunuzi na matumizi ya fedha zilizotolewa sambamba na kuangalia masuala ya utawala bora kwa kuangalia ushirikishwaji wa jamii, sheria zilitumika vipi katika kipindi chote cha utekelezaji wa mradi.

"..Kazi iliyofanyika ni nzuri na thamani ya pesa inaonekana, hakuna sababu ya kumnyima pesa mtu anaetumia vizuri naamini hata zikija fedha nyingine zitatumika ipasavyo kikubwa miundo mbinu hii ilindwe ili idumu na vizazi vijavyo vikute matunda haya.."

Nae Mkurugenzi wa elimu ya awali na msingi kutoka OR-TAMISEMI Bi.Susana Nussu amesema serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imejipanga vizuri katika kujenga na kuboresha miundo mbinu mbalimbali ya elimu.

"..Elimu ndio kipaumbele chetu, tunafahamu tunalo jukumu kubwa la kuzalisha watu watakaopambana katika soko la kimataifa kielimu bila kuwa na mazingira rafiki yanayoakisi hayo itakuwa ngumu..."

Kamani Shigella ni mkazi wa mtaa wa Kabambo yeye ni mmoja wa wajumbe katika kamati ya ujenzi wa shule ya sekondari Kisenga ameomba ujenzi unaokuja uwe wa maghorofa kwa kuzingatia ufinyu wa maeneo na kuwahakikishia wataalam hao kuwa kamati ipo tayari kusimamia mradi wowote utaoletwa kwao.

Hoja ya Shigella ya ujenzi wa maghorofa imepokelewa na timu nzima ya wataalam hao huku wakiwapa nafasi wataalam wenyeji kuanza kuchakata upatikanaji wa maeneo yasiyo na migogoro na kuyapatia hati miliki.

Shule zilizotembelewa ni pamoja na Bwiru wasichana iliyopo kata ya Pasiansi, Kisenga sekondari Kiseke ilogharimu kiasi cha shilingi 584,280,000 na shule ya msingi Buteja ilokamilika kwa jumla ya kiasi cha shilingi milioni 540.3 ndani ya kata ya Kahama.

Announcements

  • ORODHA MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO WALIOTEULIWA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI MWAKA 2025 JIMBO LA ILEMELA October 20, 2025
  • TANGAZO LA UPANGISHAJI WA VYUMBA VYA BIASHARA October 16, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -JIMBO LA ILEMELA October 14, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO 2879 WAAPISHWA,WAMEASWA KUZINGATIA SHERIA KANUNI NA MIONGOZO

    October 26, 2025
  • ILEMELA KUBORESHA LISHE MASHULENI, DC MKALIPA AKABIDHI MBEGU NA MBOLEA

    October 25, 2025
  • DC MKALIPA AMEWATAKA WATUMISHI IDARA YA AFYA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    October 24, 2025
  • KAMBI YA MADAKTARI BINGWA WA RAIS SAMIA YAANZA KUTOA HUDUMA ILEMELA

    October 20, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.