• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

AWAMU YA KWANZA UCHANJAJI MIFUGO KUANZA TAREHE 03 JULAI, KUKU ELFU 70 KUCHANJWA

Posted on: July 2nd, 2025

Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali- Ilemela

Halmashauri ya manispaa ya Ilemela inatarajia kuanza utekelezaji wa zoezi la uchanjaji wa mifugo tarehe 03 Julai 2025 zoezi ambalo litadumu kwa muda wa takriban wiki mbili ikiwa ni utekelezaji wa mkakati wa serikali wa kupunguza na kutokomeza vifo vya mifugo vitokanavyo na magonjwa ya homa ya mapafu ya ng'ombe, sotoka ya mbuzi, kideri kwa kuku, ndui na mafua makali ya kuku.


Katika manispaa ya Ilemela zoezi hili la uchanjaji litatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itahusisha uchanjaji wa kuku wa asili wanaokadiriwa kufikia elfu sabini huku awamu ya pili itahusisha uchanjaji wa ng'ombe na mbuzi sambamba na uwekaji wa hereni kwa ajili ya utambuzi na itaanza mara baada ya kupokea vifaa vingine kama friji, pikipiki sindano vishkwambi n.k

Akikabidhi chanjo hizo kwa maafisa mifugo leo tarehe 02 Julai,2025, Ndugu Petro Joseph ambae alimwakilisha kaimu mkurugenzi amesema kuwa manispaa ya Ilemela imekwishapokea chanjo  elfu 23 za ng'ombe, chanjo elfu 70 za kuku na chanjo elfu 28 za mbuzi pamoja na  baadhi ya vitendea kazi.

"Niwatake kuhakikisha kuku wote wanaofugwa ndani ya manispaa ya Ilemela wanachanjwa, sambamba na kutoa elimu kwa wafugaji ikiwa ni pamoja na kuzingatia sheria na taratibu wakati wa utekelezaji wa zoezi hili", amesisitiza Ndugu Peter


Naye Dkt. Nelson Rugaimukamu, afisa mifugo wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa chanjo hizi bure na kutoa rai kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa wataalamu wakati wa  zoezi hili  kwani itawasaidia kupunguza gharama za matibabu kwa mifugo yao na kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa yanayosababishwa na kukosekana kwa chanjo

 Akizungumza kwa niaba ya maafisa mifugo wa halmashauri Ndg. David Wanoka, afisa mifugo kata ya Kayenze amesema kuwa amezipokea chanjo hizo na  ameahidi kuwa  watahakikisha zoezi la utoaji wa chanjo hizo linafanyika kwa ufanisi katika kata zote.

Kampeni hii ya kitaifa ya chanjo na utambuzi wa mifugo ilizinduliwa rasmi na Rais Mhe Samia Suluhu Hassan Juni 16,2025 mkoani Simiyu itatekelezwa kwa miaka mitano kuanzia mwaka wa fedha 2025/2026.

MWISHO 

 

 

Announcements

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • CHANJO YA KUKU KUWANUFAISHA WAFUGAJI

    July 09, 2025
  • PROF NAGU AMEWATAKA WATUMISHI KADA YA AFYA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    July 08, 2025
  • WALIMU WA AJIRA MPYA WAMETAKIWA KUWEKA MIPANGO SAHIHI YA KAZI

    July 04, 2025
  • ELIMU YA FEDHA KUWAONGEZEA UFANISI WANUFAIKA WA TASAF

    July 03, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.