• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ASASI ZISIZO ZA KISERIKALI ZANUFAIKA NA ELIMU YA RUSHWA KUTOKA TAKUKURU

Posted on: August 12th, 2024

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Ilemela imetoa elimu ya rushwa kwa Asasi zisizo za kiserikali zinazojihusisha na sekta mbalimbali ikiwemo elimu,afya, kilimo,teknolojia ya habari na mawasiliano na haki za binadanamu zinazofanya kazi zake ndani ya Manispaa ya Ilemela ikiwa ni sehemu ya kuleta uelewa wa pamoja juu ya misingi ya utawala bora na sheria.

Akizungumza wakati wa jukwaa la asasi zisizo za kiserikali (NGOs) kujadili taarifa zao za utekelezaji katika robo ya nne ya mwaka wa fedha 2023/2024 Afisa wa TAKUKURU Bi.Doreen Ntongani amesema ni muhimu taasisi zote za umma kufahamu umuhimu wa misingi ya utawala bora.

Amefafanua kuwa taasisi za umma ni zote zinazojihusisha na utoaji wa huduma kwa jamii zinaweza kuwa za kiserikali au zisizokuwa za kiserikali na kuzitaka taasisi hizo kwa pamoja kufanya kazi kwa uwazi na uwajibikaji na kuepuka mazingira yoyote ya rushwa.

"..Rushwa ni kitu chochote cha thamani kinachotolewa kwa manufaa binafsi hasa kwa watu wenye mamlaka,kuishinda inahitaji wote tuungane na kuipinga "

Amewataka viongozi katika asasi hizo kuajiri wafanyakazi kwa uwezo wao na vigezo vinavyotakiwa na si kwa upendeleo wa namna yoyote kwa kuangalia kabila ,dini au vyuo walivyotoka huku akiwatahadharisha namna rushwa inavyoweza kuua uzalendo.

Akijibu swali la Vivian Kori Meneja wa asasi ya Fadhili Teens Tanzania alilohoji ugumu wa upatikanaji wa taarifa za taasisi za serikali Bi Doreen amesema ni haki ya kikatiba raia kupata habari na kuwataka wataalam wa asasi hizo kuhudhuria mikutano ya wazi kama vile mabaraza ya madiwani ambako taarifa zote za umma zinatolewa.

Jimmy Luhende ni Mwenyekiti wa asasi zisizo za kiserikali mkoa wa Mwanza yeye amewataka wakurugenzi wenzie kwenye asasi zao kuwa na mahusiano ya karibu na wataalam mbalimbali wa kiserikali ili kurahisisha mawasiliano baina yao.

Akihitimisha kikao hicho Msajiri wa asasi zisizo za kiserikali wilaya ya Ilemela ndugu Yusuph Onkwonkwo amezishukuru asasi zote kwa ushiriki wao huku akiwataka kuboresha zaidi taarifa zao za utendaji kutumia majukwaa ya aina hiyo kutoa maoni na mawazo mapya ili kufanya kazi zao kuwa bora zaidi.

















Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.