• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

"Anaetoa na Kupokea Rushwa wote wanafanya makosa"-Kitinga

Posted on: November 19th, 2021

Na Paschalia George na Yusuf ludimo, Ilemela


Rushwa ni adui wa maendeleo ,hivyo ni jukumu la jamii nzima kutambua ubaya wa rushwa ili iwe rahisi kuepukana nayo. “Anaetoa au kupokea rushwa wote wanafanya makosa” amesema Ndugu Said Kitinga


Ndugu Said Kitinga, ambae ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela ameyasema hayo alipomwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Ilemela katika zoezi la kuzindua muongozo wa mafunzo wa kupambana na rushwa ambayo yatahusisha wataalam wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Chama cha Skauti Tanzania ndani ya wilaya ya Ilemela.

Aliongeza kusema kuwa mambo yamekuwa hayaendi yanavyopaswa kwenda kwani jamii ikishajiaminisha kwenye uwepo wa kitu kidogo ndo chachu ya jambo fulani kufanyika kwa haraka na kwa ufanisi lazima jamii husika isue sue katika masuala ya kimaendeleo.


 ‘’ Rushwa ni adui wa haki,ni muhimu kwa jamii yetu kuwalea watoto kwa kuwapatia elimu hii juu ya madhara ya rushwa toka wakiwa wadogo wakue wakichukia na kupinga rushwa.Viongozi wenzangu bado tunao wajibu mkubwa wa kufikisha elimu kwa jamii nzima,naomba jambo hili likahusishe kila mmoja kwa nafasi yake na tukemee kuhusu adui huyu mkubwa wa maendeleo”amesema Kitinga .


Nae Kamanda wa TAKUKURU wilaya ya Ilemela Norbert Ndika amefafanua kuwa uzinduzi wa muongozo huu kwa kushirikiana na jeshi la skauti Tanzania ni mpango wa serikali wa kuendelea kusambaza elimu ya kuzuia na kupambana na rushwa kwa kutumia vijana wa skauti ambao tayari wamepitia mafunzo ya awali ya uzalendo na wanauwezo wa kuhamisha elimu hii katika makundi tofauti tofauti ndani ya jamii wanazoishi kama vile shuleni na mpaka ngazi ya kaya.

“Tunatarajia shule zetu zote ndani ya Ilemela kuwa na vikundi vya mapambano dhidi ya rushwa ndani ya shule ambapo vijana hawa watapewa mafunzo ya kupambana na rushwa elimu ambayo wao watapaswa kuifikisha kwa wenzao ndani na nje ya shule.Tunataka jamii itakayohoji matumizi mabovu ya fedha pale inapoonekana sio sahihi sambamba na kuibua makosa au vitendo viovu vinavyochochea au rushwa yenyewe.”amesema kamanda Ndika.


Rushwa imekuwa adui katika maeneo mengi hasahasa maeneo ya kutolea huduma za umma kama vile elimu ,afya na shughuli mbalimbali za kiuchumi. Uwepo wa rushwa maeneo hayo unazolotesha huduma hizo na kusababisha watumishi au wahusika kutokufanya kazi kwa weledi wao na hivyo kusubiri mpaka wapate kitu flani cha kuwanufaisha ndipo huduma itolewe.

Kamishna wa skauti wilaya ya Ilemela Jesca Ndelwa ameupokea mpango huu kwa furaha kubwa huku akiahidi ushirikiano wa kiwango cha juu kabisa katika kutoa elimu hiyo umma.


“Hatutokaa kimya kuruhusu rushwa iendelee kututawala,tutatoa elimu ya kutosha kwa vijana wetu wa skauti na wao wataitoa kwa wengine, tutaendelea kusambaza elimu hiyo kwa namna mbalimbali zenye tija kwa jamii yetu ya Ilemela”amesema Kamisha Ndelwa


Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

    June 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.