• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ALAT MWANZA YAIPONGEZA ILEMELA UJENZI WA BARABARA KWA MAPATO YA NDANI

Posted on: November 28th, 2023


Jumuiya ya mamlaka ya serikali za mitaa (ALAT) mkoa wa Mwanza imeipongeza manispaa ya Ilemela kwa kutenga fedha na kuanza ujenzi wa barabara ya hospitali ya Wilaya kwa kiwango cha lami  yenye urefu wa kilomita 1.3.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya manispaa ya Ilemela Mwenyekiti wa ALAT mkoa wa Mwanza ambae pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Magu Mhe. Mpandalume Simon amesema kuwa manispaa ya Ilemela inastahili pongezi kwa uthubutu wa kutenga fedha za mapato ya ndani na kuanza ujenzi wa barabara hiyo licha ya jukumu la usimamizi na ujenzi wake kuachiwa wakala wa barabara za mijini na vijiji (TARURA).

" ALAT mkoa wa Mwanza tunaipongeza Ilemela chini ya Mwenyekiti wake, Mkurugenzi na wataalam wote kwa kutenga fedha zaidi ya bilioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii, Bilioni moja kwa awamu ya kwanza na nyingine itatumika awamu ya pili kukamilisha mradi huu , sisi wa kutoka halmashauri nyingine tunalo la kujifunza ." Alisema

Aidha Mhe. Mpandalume amemshauri Meya wa manispaa ya Ilemela kuhakikisha anasimamia vizuri malipo ya mkandarasi anaetekeleza mradi huo ili uweze kukamilika kwa wakati.

Kwa upande wake msimamizi wa mradi huo , Mhandisi Jacob Buswege kutoka TARURA  wilaya ya Ilemela amesema kuwa mradi unatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi millioni 904.47 hadi kukamilika kwake na kuongeza kuwa utekelezaji wa mradi huo ulianza Juni 12, 2023 kupitia mkandarasi Kaserkandis Construction & Transport Co. Ltd ya mkoani Mwanza.

Nae mstahiki meya wa manispaa ya Ilemela Mhe. Renatus Mulunga amesema kuwa kufanikiwa kwa miradi inayotekelezwa ndani ya manispaa yake ni kutokana na ushirikiano mzuri uliopo kwa uongozi mzima kuanzia Mbunge wa Jimbo hilo Dkt. Angeline Mabula, Mkuu wa wilaya Mhe. Hassan Masala, Baraza la madiwani ,mkurugenzi na viongozi wa CCM.

Wajumbe wa ALAT mkoa wa Mwanza wapo wilaya ya Ilemela kwa wa ziara ya siku mbili ambapo miradi mingine  iliyotembelewa ni ujenzi  wodi katika hospitali ya Wilaya ya Ilemela Sangabuye na ujenzi wa shule mpya ya msingi Butuja iliyopo kata ya Kahama.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.