• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
      • Mikakati ya MSM
    • Mikakati ya MSM
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo Cha Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha ukaguzi wa ndani
      • Kiengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Uhusiano na TEHAMA
    • Kata
      • Sangabuye
      • Nyasaka
      • Buswelu
      • Nyamhongolo
      • Kayenze
      • Bugogwa
      • Shibula
      • Ilemela
      • Kahama
      • Kiseke
      • Pasiansi
      • Kawekamo
      • Ibungilo
      • Nyamanoro
      • Buzuruga
      • Mecco
      • Nyakato
      • Kirumba
      • Kitangiri
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Uvuvi
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Michezo
  • Huduma zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya wah. wabunge na madiwani
    • Kamati za kudumu za halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • MipangoMiji na Mazingira
      • Uchumi Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi Iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba

Wataalam wa elimu, afya na ustawi wa jamii wajengewa uwezo wa kupambana na vitendo vya ukatili

Posted on: February 23rd, 2021

Wataalam wa elimu, afya na ustawi wa jamii katika Manispaa ya Ilemela wamejengewa uwezo wa kubaini, kuchukua hatua na kupambana na vitendo vya ukatili, ulinzi na usalama kwa watoto wenye umri wa kuanzia miaka tisa hadi kumi na nne kupitia vipindi vya michezo na dini mashuleni.
Mafunzo hayo yamelenga kuwaanda vijana kuwa wanaume bora ‘Coaching Boys Into Men’ CBIM kupitia mradi wa BORESHA ili waweze kutambua na kuheshimu haki zao na za watu wengine pamoja kupinga vitendo vya kikatili na unyanyasaji kwa ajili ya kujenga jamii iliyo sawa na yenye kuwajibika

Akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu hao, afisa elimu michezo wa Manispaa ya Ilemela Mwalimu Kizito Bahati Sosho alisema  kuwa wanafunzi watakapopata ufahamu juu ya vitendo vya kinyanyasaji na ukatili itawasaidia wao kujilinda na kuvipinga vitendo hivyo.

‘.. Tunategemea wanafunzi wetu watakapopata ufahamu juu ya vitendo vya kinyanyasaji na ukatili itasaidia wao wenyewe kuchukua hatua za kupinga vitendo hivi vya kinyanyasaji kwao wenyewe na kwa watu wengine ..’ Alisema



Aidha afisa ustawi wa jamii wa Manispaa ya Ilemela Bi Stella Mbura akaongeza kuwa Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kudhibiti vitendo vya ukatili kwa watoto na unyanyasaji ikiwemo kuanzisha timu za ulinzi na usalama wa watoto (MTAKUWWA) kwa ngazi ya mitaa, kata na wilaya.
Pamoja na jitihada hizo alisema kuwa zipo ofisi za ustawi wa jamii ambazo hutumika kwa ajili ya kutoa taarifa matukio mbalimbali ya kikatili na unyanyasaji huku wakishirikiana na vituo vya polisi kupitia dawati la jinsia na watoto na mashirika mbalimbali ambayo husaidia kutoa msaada wa kisheria pamoja na elimu ya kuzuia matendo ya aina hiyo.

Kwa upande wake mratibu mwandamizi kutoka shirika la TIP (Tanzania Interfaith Partnership) Ndugu Shukuru Mohammed alisema kuwa mradi wa BORESHA unatekelezwa katika wilaya tatu za Ilemela, Kwimba na Buchosa mkoani Mwanza huku ukitekeleza afua ya UKIMWI ambapo una vipaumbele viwili cha kwanza ni kuhimiza wakinababa na wavulana kupima ili kujua hali zao za kiafya na ya pili ni kumlinda mtoto kwa maana ya watu wenye umri chini ya miaka 18 ambapo afua hizi kubwa mbili zimebeba afua ndogo ndogo ikiwemo afua ya mafunzo ya kumfanya mvulana kuwa mwanaume bora ‘Coaching Boys Into Men’ CBIM.
Aliongeza kuwa afua hii imekusudia kumjengea mtoto uwezo wa kujitambua nafasi yake kuwa mtu mzima na kuthamini usawa wa kijinsia ambapo afua hii itaendeshwa kupitia vipindi vya dini na michezo vya kila wiki mashuleni kwa wanafunzi wa kiume kuwekwa katika makundi ya idadi ya watoto arobaini wakifundishwa namna ya kujiepusha na kuripoti vitendo vya ukatili, unyanyasaji wa kijinsia na baadae kushiriki michezo kwa pamoja vyote vikibeba dhima ya kupambana na ukatili.

Nae moja ya washiriki wa mafunzo hayo Mwalimu Frida Mollel kutoka shule ya msingi Kirumba iliyopo kata ya Kirumba akaishukuru serikali na shirika la kijamii la TIP kwa kuja na mpango huu wa mafunzo ya kuwaanda vijana kuwa wanaume bora kwani utawasaidia kujitambua hivyo kupunguza vitendo vya ukatili na unyanyasaji katika jamii
Mafunzo haya yameendeshwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali ya TIP, AGPAHI na WORLD VISION kwa mafunzo kwa baadhi ya maafisa wa idara ya elimu msingi, ustawi wa jamii, afya na walimu wa shule 35 zilizopo ndani ya wilaya hiyo, shule 30 zikiwa za Serikali na shule 5 zinazomilikiwa na watu binafsi.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA YA KAZI MTENDAJI WA MTAA March 03, 2021
  • Matokeo Darasa la Saba2020 November 23, 2020
  • Orodha ya Majina ya wanafunzi wavulana na wasichana waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2021 shule za kutwa December 19, 2020
  • Orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2021 -Mahitaji maalum December 19, 2020
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Mganga Mkuu Ilemela awataka wadau kuendelea kuunga mkono jithada za serikali

    April 15, 2021
  • Wananfunzi wajengewa uwezo kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji

    March 09, 2021
  • Mgogoro wa ardhi Kigoto wahitimishwa rasmi

    March 04, 2021
  • Wataalam wa elimu, afya na ustawi wa jamii wajengewa uwezo wa kupambana na vitendo vya ukatili

    February 23, 2021
  • Angalia zote

Video

Madiwani Ilemela waapishwa /wampata meya wao
Video zaidi

Ukurasa wa Karibu

  • Kuhakiki Taarifa za Mpiga Kura
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip
  • Maombi ya leseni ya biashara

Kurasa zinazofanana

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza
  • Tovuti Kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Anuani ya Posta: 735 MWANZA

    Simu: + 255 736 200910

    Simu:

    Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki 2019 Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela.Haki zote zimeifadhiwa