• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

Posted on: April 30th, 2025

Wananchi wa Jimbo la Ilemela wametakiwa kutumia fursa ya uwekaji wazi wa daftari la awali la wapiga kura kwa ajili ya kuhakiki taarifa zao ambapo zoezi hili litaenda sambamba na uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili litakaloanza tarehe 01 Mei hadi 07 Mei 2025.

 

Afisa Mwandikishaji wa jimbo la Ilemela Bi Ummy Wayayu alitoa rai hiyo wakati akifungua mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili yaliyoendeshwa na tume huru ya taifa ya uchaguzi siku ya tarehe 29 Aprili 2025 kwa waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki

 

“Nitoe rai kwa wananchi wote wa Ilemela kuhakikisha wanatumia fursa hii kwa kupita kwenye vituo vilivyoainishwa katika kata zao ili waweze kulikagua daftari hilo, kufanya marekebisho ya taarifa zao, kuingiza au kufuta majina ya wapiga kura pamoja na kuweka pingamizi kwa mpiga kura aliyeandikishwa na hana sifa za kuwemo kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ili kuweza kushiriki uchaguzi mkuu”. Alisema Bi Ummy

 

Mafunzo hayo yalitanguliwa na uapisho kwa washiriki wa mafunzo hayo kwa ajili ya kujitoa kwenye vyama vya siasa na utunzaji wa siri ambapo yalienda sambamba na mafunzo kwa vitendo ya mfumo wa uandikishaji na vifaa vya BVR pamoja na ujazaji wa fomu lengo likiwa ni kuwajengea umahiri wa kutekeleza zoezi hilo na kuhakikisha zoezi la uboreshaji linakamilika kwa ufanisi. 

 

Bi Ummy aliwahimiza ushirikiano mzuri na wa karibu na Tume wakati wa zoezi hili na kuwasisitiza wanazingatia muda wa kufungua vituo ambao ni saa mbili kamili asubuhi kwani asingependa kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi pamoja na kuwasikiliza na kuwapa ushauri yanayopaswa kufanyika bila kutumia nguvu.

 

 “Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili ni maandalizi ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi wa kumi 2025, na hii ni kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ambapo inaitaka tume huru ya taifa kufanya uboreshaji mara mbili kati ya uchaguzi uliomalizika na kabla ya siku ya uteuzi”, alibainisha afisa uchaguzi wa Ilemela Ndugu Shilinde Malyagili.

 

 

Mohammed Maarufu afisa mwandikishaji msaidizi ngazi ya kata aliyekuwa mwenyekiti wa mafunzo hayo alimhakikishia Afisa Mwandikishaji Jimbo kuwa wamezingatia na kuyaelewa yote waliyoelekezwa na kufundishwa na kuyachukua na kuwa wako tayari kutekeleza kazi  hiyo maalum.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.