• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

WAFANYABIASHARA ILEMELA WATAKIWA KUFUATA BEI ELEKEZI UUZAJI WA SARUJI

Posted on: December 1st, 2020

Wafanyabishara wilayani Ilemela wametakiwa kuzingatia bei elekezi ya Serikali katika uuzaji wa saruji kwa wananchi na Serikali haitamvumilia mfanya biashara yeyote atakaeenda kinyume na agizo hilo kwa kuuza bidhaa hiyo kwa zaidi ya shilingi elfu kumi na tisa na mia tano.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe Dkt Mathias Severine Lalika alipofanya ziara ya kufuatilia upatikanaji wa saruji, zoezi la uuzaji linavyoendeshwa kwa wafanya biashara wa jumla na rejareja na uzingatiaji wa sheria, miongozo na taratibu za Serikali kwa wafanya biashara wa bidhaa hiyo ambapo amekemea upandishaji holela wa bei ya bidhaa hiyo bila kuwepo kwa sababu za msingi kwani Serikali imekuwa ikitoa neema tofauti tofauti kwa wafanyabiashara wakubwa wanaochukua saruji moja kwa moja kiwandani ikiwemo kuweka kodi rafiki na kuchukua mzigo bila fedha taslimu mkononi ili waweze kuuza kwa gharama nafuu kwa wananchi


‘.. Ziara hii  ni utekelezaji wa agizo la Serikali kupitia Mheshimiwa Waziri Mkuu alilotoa hivi karibuni kupitia Wakuu wa Mikoa baada ya kuongezeka kwa bei ya saruji hapa nchini ghafla, Kwa hiyo Sisi Ilemela tumewaelekeza bei ya ukomo isizidi 19,500 kwa wananchi ..’ Alisema


Aidha Mkuu huyo wa wilaya akawahakikishia wananchi ndani ya wilaya hiyo kuwa Saruji ipo ya kutosha kukidhi mahitaji yao huku akisisitiza kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Mhe Dkt John Magufuli inawapenda wafanya biashara na ipo tayari kuendelea kushirikiana nao katika ustawi wa nchi pamoja na kuwalinda wananchi wanyonge wanaotumia bidhaa hiyo


Kwa upande wake katibu tawala wa wilaya ya Ilemela Ndugu Saidi Kitinga akashauri wafanyabiashara hao kuzingatia bei elekezi ya Serikali kwani kwa kufanya hivyo itawasaidia kuongeza mzunguko wa biashara na faida hivyo kuleta tija kwa pande zote kwa maana ya wao binafsi, Serikali na wananchi kwa ujumla

Nae afisa biashara kutoka Manispaa ya Ilemela Bi Bertha George mbali na kusisitiza juu ya kuzingatia bei elekezi ya uuzaji wa saruji katika soko akapongeza wafanya biashara hao kwa kuwa na nyaraka halali za ufanyaji biashara ikiwemo leseni ya biashara na namba ya mlipa kodi, Huku afisa kutoka mamlaka ya mapato na kodi nchini TRA Bwana Rogati Joseph akihitimisha kwa kusema kuwa katika ziara hiyo amebaini upandishaji holela wa bei ya bidhaa hiyo huku akiwataka wafanya biashara wote wanaouza saruji kinyume na maelekezo ya Serikali yaliyotolewa na mkuu wa wilaya kuacha tabia hiyo mara moja kwani baada ya hapo hakutakuwa na huruma kwa mtu yeyote atakaekaidi agizo lililotolewa.

Akihitimisha mfanyabiashara Bi Khadija Said kutoka Texas Hardware ambae ndio wakala mkuu wa bidhaa ya saruji ndani ya wilaya ya Ilemela mbali na kushukuru kwa elimu aliyoipata kufuatia ziara hiyo ya kamati ya ulinzi na usalama akaahidi kuzingatia bei elekezi ya bidhaa hiyo kwa wateja wake sanjari na kuwasisitiza nao kuzingatia maelekezo ya serikali wanapoenda kuuza kwa watumiaji wa mwisho.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.