• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

SUALA LA UPANDAJI MITI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA LIWE ENDELEVU

Posted on: December 10th, 2024

Kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu wake kwa kutambua umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti ili kupambana na mabadiliko ya tabianchi yanayoendelea kuleta madhara makubwa duniani kwa sasa.

Hayo yamezungumzwa na mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Cde.Christopher Ngubiagai wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Mwanza kwenye viwanja vya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela katika maadhimisho ya miaka 63 ya uhuru wa Tanzania bara yanayoadhimishwa nchini kila tarehe 09 Desemba ya kila mwaka tangu nchi hiyo ilipopata uhuru mnamo mwaka 1961.

“..Uhuru ni haki ya msingi ya kila mtu au taifa kuamua kufanya mambo bila kuingiliwa na mtu yoyote ki maamuzi…” Amesema Cde.Ngubiagai akimnukuu hayati baba wa taifa la Tanzania Mwl.Julius Kambarage Nyerere

Cde.Ngubiagai ameongeza kuwa pamoja na shughuli mbalimbali ambazo zinafanyika katika maadhimisho hayo ni muhimu kuwaenzi waasisi wa taifa kwa kuzingatia misingi ya uhuru ambayo inajumuisha umoja,usawa,uwajibikaji,kujitegemea na haki za binadamu ili kuleta maendeleo kwa kasi.

“..Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri anayoendelea nayo ya kuleta maendeleo,kipindi cha uhuru mkoa wa Mwanza ulikuwa na shule 5 tu leo tuna jumla ya shule 332 na nyingine zinaendelea kujengwa..”

Aidha Afisa usalama mstaafu wa mkoa wa Mwanza Dkt.Jason Mutashi ametoa mada kuhusu amani wakati wa kongamano lililojikita zaidi katika masuala ya uhuru wa Tanzania bara, amesema nchi hiyo ilipata uhuru wake kwa njia ya amani bila kumwaga damu na kwamba nchi iliongozwa kwa kufuata misingi ya amani ,umoja na uadilifu bila kujali dini wala makabila ya mwananchi wake.

“.. Hatuna budi kuilinda tunu ya taifa letu ambayo ni amani..” amesema Dkt.Mutashi

Nae Mkuu wa Wilaya ya Ilemela mstaafu Dkt.Leonard Masale amesema Tanzania bara inatimiza miaka 62 ya jamhuri huku akifafanua maana jamhuri kuwa ni jamii huru

“..Nyakati za nyuma hali ya maendeleo haikuwa nzuri,sekta ya elimu ,afya miundo mbinu ya barabara ilikuwa duni sana ndo kisa cha hayati baba wa taifa Mwl.Nyerere kuanzisha vita dhidi ya maadui watatu ambao ni maradhi ,umaskini na ujinga ,vita ilozaa matunda chanya tunayoyaona leo..”

Hoja Misong’hwani ni mwenyekiti wa mtaa wa Kadinda katika kata ya Kahama ndani ya Manispaa ya Ilemela yeye anasema kumekuwa na maendeleo mengi makubwa mtaani kwake akilinganisha na hali ilivyokuwa wakati wa uhuru huku akikiri kuwepo kwa huduma za maji na umeme kwenye mtaa wake vitu ambavyo havikuwepo awali.

Maadhimisho hayo yamepambwa na kauli mbiu isemayo uongozi madhubuti na ushirikishwaji wa wananchi ni msingi wa maendeleo yetu.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.