• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MWENYEKITI UWT (T) ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA

Posted on: August 12th, 2024

Ndugu Mary Chatanda, ambae ni Mwenyekiti wa UWT Taifa ameridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa wilayani Ilemela. Amebainisha hayo akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humu yenye lengo la kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya CCM sambamba na kulinganisha thamani ya fedha iliyotumika katika miradi hiyo.

Akiwa wilayani Ilemela amekagua bweni la wasichana katika shule ya sekondari ya Bwiru lililojengwa kwa fedha za mradi wa SEQUIP kiasi cha Shilingi milioni 130 pamoja na Shule mpya ya Sekondari ya Kisenga iliyopo kata ya Kiseke iliyojengwa kwa fedha za EP4R kiasi cha Shilingi Milioni ambapo amepongeza jitihada za serikali na kuelekeza miundombinu hiyo ya shule kutunzwa.

Sambamba na ukaguzi wa miradi ya elimu alikagua ujenzi wa barabara ya Buswelu Nyamadoke Nyamhongolo (km 9.5) inayojengwa kwa fedha kutoka benki ya dunia, ambapo Ndugu Chatanda amemtaka mkandarasi kuhakikisha anaijenga barabara hiyo kwa viwango na kuikamilisha kwa wakati uliopangwa ili kukidhi mahitaji ya wananchi.

Ndugu Chatanda katika nyakati tofauti alipata wasaa wa kuwahutubia wanachi wa kata za Pasiansi, Kitangiri na Kawekamo ambapo alisisitiza juu ya suala la kuporomoka kwa maadili na kuwataka wazazi kuhakikisha wanawasimamia wao na kushirikiana na walimu katika malezi hayo huku akiwataka watoto wa kiume na wa kike kuhakikisha wanazingatia masomo na kuachana na mambo ya kidunia.

Kuhusu mikopo ya asilimia 10 ya halmashauri amemuelekeza Mkurugenzi kuhakikisha maafisa maendeleo ya jamii kutoa mafunzo ya matumizi bora ya mikopo kabla ya kutoa mikopo kwa walengwa ili mikopo hiyo ilete tija kwao.

Sambamba na hayo Ndugu Chatanda amewataka wana Ilemela kuhakikisha wanashiriki zoezi la uboreshaji wa taarifa katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu 2025.

Nae mbunge wa jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula amemuomba ndugu Chatanda kufikisha salam za shukrani kwa Rais Samia kwa fedha nyingi alizotoa jimboni humo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi akizitaja kuwa ni takribani shilingi bilioni 69 zimepokelewa katika kipindi cha miaka mitatu.

Ziara hiyo imejumuisha wajumbe wa kamati ya utekelezaji ya Baraza kuu Taifa na viongozi mbalimbali wa UWT ambapo nao walipata wasaa wakukagua miradi katika kata mbalimbali ndani ya wilaya ya Ilemela ikihusisha miradi ya sekta za Afya, elimu na miundombinu ya Barabara.




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.