• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMATI YA UKIMWI ILEMELA YAWATAKA WAHUDUMU KUTOA HUDUMA NZURI

Posted on: October 18th, 2022

Kamati ya Kudhibiti UKIMWI ya Manispaa ya Ilemela imewataka wahudumu wa afya kutoa huduma nzuri na za viwango vinavyotakiwa kwa wateja wao hayo yamesemwa wakati wa ziara ya kukagua zahanati zinazotoa huduma na ushauri nasaha kwa walioathirika na ugonjwa wa UKIMWI.


Katika ziara hiyo, kamati hiyo ilipokea taarifa za zahanati hizo za Ilemela,Pasiansi na Buswelu zilizoainisha huduma zinazotolewa ikiwemo ushauri nasaha na kupima VVU,huduma ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto,huduma ya uangalizi na matibabu ya kufubaza maambukizi ya VVU sambamba na kuzalisha kina mama wajawazito.

Aidha taarifa hiyo ilitaja mafanikio katika huduma za UKIMWI zinatolewa ikiwemo ongezeko la madawa na vitenganishi kutoka serikalini na wadau wa ICAP wanaojishughulisha na masuala mbalimbali ya afya ikiwemo UKIMWI.Kuweza kutoa huduma za mkoba na kuweza kuibua watu wapya wenye maambukizi na kuwapa huduma stahiki.


Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe.Sadick Manusura akiwaongoza wajumbe wa kamati hiyo amesema kuwa jamii nzima inao wajibu wa kuwajali waathirika na kuungana katika kuboresha huduma za UKIMWI huku akikiri kuzitambua changamoto mbalimbali zinazowakabili na kuahidi kuzitafutia ufumbuzi.


 “ Jamii nzima tunaowajibu wa kuwajali watu hawa kwa kuungana katika maboresho ya huduma za UKIMWI tukianza na kuboresha na kujenga vituo bora vya kutolewa huduma hizi maalum kwa wenzetu walioathirika kwa kutambua kuwa janga hili ni letu sote ”. Amesema Mhe.Manusura


Daktari Samson Marwa ambae ni Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilemela ameiasa jamii ya Ilemela kuacha kufanya ngono zembe kwani ndio  njia kuu ya kupata maambukizi ya VVU.

“ Zipo njia nyingi za kupata maambukizi, kutumia pamoja vitu vyenye ncha kali vilivyotumiwa na mtu mwenye maambukizi,mtoto kupata maambukizi wakati wa kuzaliwa lakini njia kubwa kabisa ni kufanya ngono zembe. Hivyo tuache ” Amesema Dkt.Marwa.


Nae Mhe. Juma Wesa mjumbe wa kamati hiyo amesisitiza elimu ya UKIMWI iendelee kutolewa kwa makundi mbalimbali ndani ya Manispaa ya Ilemela ikiwemo makundi ya wanaotumia madawa ya kulevya kwani hata wao ni rahisi kupata maambukizi na kushindwa kujimudu kimaisha wakiachwa na upweke.


Baadhi ya wagonjwa wa VVU wanaohudhuria kliniki katika zahanati hizo wamefurahishwa na utaratibu huo wa Manispaa ya Ilemela kutembelea na kufuatilia kwa karibu huduma za UKIMWI zinavyotolewa na kuendelea kupambana na changamoto zilizopo.              

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.