• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAENDELEA KUTEKELEZA AGIZO LA WAZIRI WA ARDHI

Posted on: May 26th, 2017

ILEMELA YAENDELEA KUTEKELEZA AGIZO LA WAZIRI WA ARDHI 

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imeendelea kutekeleza kwa vitendo agizo la waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Mheshimiwa William Lukuvi alilolitoa mapema Septemba,2017 la kuhakikisha kuwa manispaa inashirikisha wananchi katika upimaji wa maeneo ya taasisi na kuilinda mipaka ya maeneo hayo.

Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mheshimiwa Daktari Leonard Masale amewataka viongozi wa mitaa kutoa ushirikiano kwa wataalamu wa ardhi sambamba na kusisitiza juu ya utendaji wa haki katika zoezi hilo kwa kuzingatia maelekezo ya waziri wa ardhi Viongozi wenzangu wa mitaa niwaombe mkatoe ushirikiano kwa wataalamu wetu wanapokuja maeneo yenu mkumbuke kuwa wote tuna ajenda ya pamoja, 

Tukahakikishe usalama wao na kuwaelemisha wananchi wetu pale inapotokea sintofahamu ya namna yeyote ile na wataalamu niwaombe mkatende haki kwa kuzingatia maelekezo ya mheshimiwa waziri wa ardhi , sheria na taratibu”, Alisisitiza hayo katika kikao kilichoketi kwa ajili ya kuandaa utaratibu bora wa kumilikishwa viwanja hivyo baada ya zoezi la upimaji.

Nae Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela ndugu John Wanga kupitia kikao hicho ameisisitiza timu ya wataalamu inayoendelea kuongeza juhudi ili kuweza kukamilisha zoezi hilo huku akiwataka viongozi wa mitaa kusaidia serikali katika kuyalinda maeneo yote ya umma yasivamiwe.

Kwa upande wao wenyeviti wa mitaa hiyo na wazee mashuhuri wamemuhakikishia mkuu wa wilaya na mkurugenzi ushirikiano kwa wataalamu wanaoendelea na zoezi hilo na kuhakikisha wanayalinda maeneo ya umma yasivamiwe. 

Nae afisa mipango miji ndugu Francis Mwanga amebainisha hatua mbalimbali zilizofikiwa katika kuhakikisha maeneo ya taasisi yanainishwa, kupimwa, kumilikishwa na kulindwa ikiwemo kuunda kamati ambayo imeshirikiana na kitengo cha mipango miji kuandaa mpango wa maeneo, kutambua maendelezo ili kuyajumuisha katika mchoro wa mipango miji, kuandaa mchoro wa mipango miji unaojumuisha maeneo ya taasisi, kuidhinisha mpango katika ngazi zote, kufanya upimaji wa mpango, kufanya ukaguzi wa viwanja na baadae kumilikishwa. 

Kikao hicho kilijumuisha watu mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi , wataalamu wa ardhi wa Manispaa , ofisi ya ardhi kanda ya ziwa, wazee mashuhuri na viongozi wa mitaa ya Bwiru Elimu na Bwiru Ziwani.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.