• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

DC ILEMELA AKABIDHI KADI 1200 ZA BIMA YA AFYA ILIYOBORESHWA

Posted on: July 10th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Mathias Severine Lalika amekabidhi jumla ya kadi 1200 za bima za afya iliyoboreshwa kwa wanachama wa chama cha madereva na makondakta mkoa wa Mwanza(MWAREDDA) pamoja na familia zao.


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mhe.Lalika amesema madereva na makondakta ni kundi linalopaswa kuheshimiwa katika jamii kwani shughuli wanazofanya zinawezesha watu kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa haraka na ni shughuli inayochochea ukuaji wa uchumi kwa namna tofauti.

“Nawapongeza MWAREDDA kwa maamuzi mazuri waliochukua katika kujali usalama na afya zao lakini pia ni kitendo kinachounga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano ya Mhe .John Pombe Magufuli inayohamasisha wananchi wake kuwa na bima za afya ili wapate huduma hizo kwa haraka na ukamilifu pindi zinapohitajika bila kujali hali ya kifedha anayoweza kuwa nayo mwananchi kwa wakati husika”amesema .


Aidha Mhe.Lalika amewataka MWAREDDA na wananchi wengine kwa ujumla kutambua kwamba unapokuwa na kadi ya bima ya afya ni mkombozi kwako kwani una uhakika wa kupata matibabu muda wowote .


Nae mratibu wa mfuko wa iCHF wilaya ya Ilemela ndugu Leornard amefafanua kwa kina namna ambavyo mfuko unavyofanya kazi na kusema kuwa, malipo yake ni Shilingi elfu thelathini tu kwa mwaka kwa kaya ambayo itajumuisha wanafamilia sita.


“Huduma hii ni nafuu,tujiunge kwa wingi kwani uwingi wetu ndio maboresho ya huduma bora zaidi. Wanufaika wa TASAF , wanavikundi mbalimbali mnakaribishwa kujiunga na bima hii ya afya kwani ni msaada mkubwa kwetu, alisisitiza.


Nae Mwenyekiti wa chama cha madereva na makondakta Mwanza ndugu Mjarifu K.Manyasi amewapongeza wanachama wake kwa kujiunga ma bima ya afya iliyoboreshwa.


“Napongeza umoja wetu kwa ujumla kwani umekuwa wenye tija kubwa,nasisitiza umoja,mshikamano udumu ili tuendelee kupiga hatua kubwa zaidi.Tunakumbuka kwamba malengo ya umoja wetu ilikuwa ni kusaidiana katika kutatua changamoto mbalimbali za kijamii lakini sasa hivi tumeingia katika masuala ya afya”, Alisema


Akijibu changamoto ya madereva kutokuwa na mikataba ya kazi iliyotajwa katika risala ya MWAREDDA Mhe.Lalika amesema sheria ya nchi inataka watumishi wote kuwa na mikataba kwani ndio dira ya kazi mhusika anayokwenda kufanya.Mishahara ni lazima iendane na hali halisi ya maisha.

Aidha Mhe DC amewataka madereva kufata sheria na taratibu zilizowekwa bila shuruti katika kujiepusha na changamoto ya kutozwa faini za mara kwa mara pindi wawapo barabarani.


Pamoja na hayo, Mhe.Lalika ametoa tahadhari kwa wananchi wa Wilaya ya Ilemela kuendelea kujikinga na ugonjwa wa Korona kwa kufuata maelekezo ya wataalam wa afya,kunawa mikono na maji tiririka,kujiepusha na misongamano isiyokuwa ya lazima na kuvaa barakoa katika maeneo ya mikusanyiko.


Jumla ya kaya 200 zenye jumla ya wanachama 1200 wa MWAREDDA zimekabidhiwa kadi leo, ambapo mchakato wa kupata bima za afya ulianza mwezi Juni baada ya wataalam wa afya wa manispaa ya Ilemela kuwaelimisha MWAREDDA na wao kupokea kwa vitendo.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.