• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BWIRU WAVULANA YAPONGEZWA KWA KUTOKOMEZA SIFURI

Posted on: October 12th, 2023

Shule ya sekondari ya wavulana Bwiru imepongezwa kwa mipango, mikakati na juhudi ilizoweka na kufanikiwa kufuta alama sifuri katika matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2022


Pongezi hizo zimetolewa na meneja wa chuo cha elimu ya biashara tawi la Mwanza Bi Evelyne Manambo wakati wa sherehe za mahafali ya 83 ya kidato cha nne 2023 yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari Bwiru wavulana ambapo ameupongeza uongozi wa shule hiyo kwa kupata matokeo mazuri pamoja na kuwataka kuhakikisha wanafunzi wanaosoma shule hiyo wanapata daraja la tatu, la pili na la kwanza pekee katika matokeo ya miaka yote inakayofuata


‘.. Nipongeze kwa jitihada za kutokomeza sifuri, Tuhame kwenye kuondoa sifuri twende kwenye kuondoa daraja la nne, Kama huku tumeweza naamini na hili pia tutaliweza ..’ Alisema

Aidha Bi Manambo amepongeza nidhamu nzuri ya wanafunzi wa shule hiyo sanjari na kuwataka wazazi kuhakikisha wanafunzi hao wanaendelea kuwa na nidhamu katika kipindi chote watakapokuwa nyumbani mara baada ya kumaliza mitihani yao wakisubiria kwenda hatua inayofuata


Kwa upande wake mwakilishi wa mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela ambae pia ni afisa elimu taaluma sekondari Mwalimu Alex Mkusa ameishukuru Serikali chini ya Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hasan kwa kutoa fedha kwaajili ya kurekebisha miundombinu ya shule hiyo pamoja na kumpongeza mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela kwa kutoa motisha ya milioni tano kwa shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2022 huku akiwataka wazazi kulinda afya za wanafunzi katika kipindi chote watakapokuwa nyumbani


Nae mkuu wa shule ya Bwiru wavulana Mwalimu Thomas Werema akiwasilisha taarifa fupi ya shule hiyo amesema kuwa jumla ya wanafunzi 181 kati ya  211 walioanza kidato cha kwanza mwaka 2020 wameshiriki mahafali ya 83 huku wengine wakishindwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro, kuhama na kukariri darasa na kwamba shule ya Bwiru inakabiliwa na changamoto kuu mbili ambazo ni ukosefu wa vifaa vya kuhifadhia maji pamoja na mashine ya kudurufu huku changamoto nyenginezo Serikali inaendelea kuzitatua

Nazir Valentine ni miongoni mwa wahitimu wa kidato cha nne katika shule ya wavulana Bwiru mbali na kushukuru kwa kumaliza salama shule ameahidi matokeo mazuri katika mtihani wanaotarajia kuufanya hivi karibu sambamba na kuwaasa wanafunzi wenzake kwenda kuyaishi yale yote mazuri waliofundishwa wakati wakiwa shuleni


Katika mahafali hayo mgeni rasmi, meneja wa chuo cha CBE tawi la Mwanza ameahidi ununuzi wa mashine ya kudurufu na kuchapa yenye thamani ya kiasi cha shilingi milioni moja.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.