• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

BARAZA LA MADIWANI LAKUTANA NA TARURA KUJADILI CHANGAMOTO YA BARABARA ZA ILEMELA

Posted on: November 15th, 2022

Baraza la Madiwani Ilemela limekutana na TARURA Wilaya ya Ilemela  kwa ajili ya kujadili ajenda moja ya mustakabali wa barabara zinazopatikana katika Manispaa ya Ilemela

Wakiwasilisha hoja zao juu ya barabara zinazopatikana katika kata zao waheshimiwa madiwani katika nyakati tofauti, mbali na kuipongeza TARURA kwa jitihada zake wameitaka kuhakikisha kuwa barabara zote za Manispaa ya Ilemela zinawekwa katika mpango wa matengenezo na zinatengenezwa kwa viwango cha mawe au zege ili ziweze kudumu.


Pamoja na hilo wameitaka TARURA kuhakikisha kuwa wanatengeneza mitaro na makalavati imara ili kuwezesha barabara hizo kudumu na zisiharibiwe na mvua zinazoendelea huku wakiwataka kukamilisha barabara hizo kwa wakati na ili zipitike katika nyakati zote.

Aidha wameitaka TARURA kuhakikisha barabara ambazo zinaelekea katika taasisi mbalimbali kama shule hospitali na zingine kuhakikisha zinapewa kipaumbele kwani ndipo sehemu wananchi huenda kupata huduma za kijamii.


Mhandisi Sobe Makonyo kutoka TARURA akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa matengenezo ya barabara Wilaya ya Ilemela amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya mikataba 9 ya utengenezaji wa barabara inatarajiwa kutekelezwa na hadi sasa mikataba 7 imeshaingiwa kati ya miradi hiyo saba miradi miwili imekamilika, miradi 5 inaendelea na miradi miwili ipo hatua ya manunuzi.


Ameongeza kusema kuwa TARURA Wilaya ya Ilemela  imetenga kiasi cha shilingi  Bilioni 2.6 katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya matengenezo ya barabara ambapo Shilingi Bilioni 1.6 ni kutoka bodi ya barabara, Milioni 500 ni fedha za mfuko wa Jimbo  na Shilingi Bilioni moja ni fedha za tozo za mafuta na kuongeza kuwa hadi sasa fedha iliyoidhinishwa ni kiasi cha Shilingi Milioni 500 .


Nae Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Apolinary amesema kuwa Ilemela imetenga kiasi cha Shilingi Bilioni 1.2 itakayotoka katika mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili ya matengenezo ya barabara ikiwa ni maelekezo ya Serikali kuu ya kuzitaka halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya barabara.


Mhe Renatus Mulunga, Mstahiki Meya wa Ilemela ameishauri TARURA kutengeneza barabara za mawe na mitaro imara kutokana na kuwa kata nyingi zipo kwenye mwinuko ili ziweze kudumu na thamani ya fedha ionekane.huku akihimiza usimamizi mzuri na juhudi katika matengenezo ya barabara hizo.


“Niwatake TARURA kuanza kufikiria kutengeneza barabara za mawe ili ziweze kudumu muda mrefu kwani kata nyingi za Manispaa ya Ilemela zipo kwenye mwinuko”amesema Mhe Mulunga


Pamoja na hayo Mstahiki Meya, amemtaka Mkurugenzi na wataalam wote kuhakikisha wanatilia mkazo suala la ukusanyaji wa mapato ili kuwezesha upatikanaji wa shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na kusisitiza kuwa fedha hiyo itatolewa katika kata zote kwa uwiano sawa ambapo amewataka Madiwani kuainisha barabara chache ili zitengenezwe katika ubora na thamani ya fedha iweze kuonekana.


“Tumepitisha kwa kauli moja kuwa kupitia fedha hizo za mapato ya ndani kila kata itapata fedha kiasi cha Shilingi milioni 63 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na hivyo niwashauri madiwani watengeneze barabara chache ili thamani ya fedha iweze kuonekana”, Amesisitiza Mhe Mulunga


Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela inao mtandao wa barabara wa Km 875.75 Barabara za lami ni Km 35.26, zege Km 1.52, mawe Km 2.07, Changarawe km 60.18, Udongo km 776.83


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Halmashauri Ya Manispaa ya Ilemela.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.